Saturday, July 28, 2007

WASIFU WA ALI MWINYI MSUKO

CURICULUM VITAE

JINA KAMILI: Ali Mwinyi Msuko
TAREHE YA KUZALIWA: 01.01.1960
MAHALI PAKUZALIWA:
KIJIJI: Mitakawani
WILAYA: Kati
MKOA: Kusini Unguja

ELIMU
· MSINGI: 1966 – 1973 Skuli ya Uzini
· SEKONDARI YA AWALI: 1974 – 1976 Skuli ya Uzini
· CHETI CHA KIDATU CHA IV 1979 Privet
· CHETI CHA UALIMU DARJA III A: 1980 – 1982 Nkurumah
· STASHAHADA YA SAYANSI YA JAMII: 1985 – 1986 Higher Komsomol School Moscow USSR
· MAFUNZO YA SIASA NA ULINZI: 1976 Kambi ya Viana U/Ukuu
· MAFUNZO YA MAKADA WA KUSUKUMA MBELE MAPINDUZI YA KILIMO: 1988 Chuo cha CC M Zanzibar
· MFUNZO YA UALIMU WA VIJANA NA CIPUKIZI:
1979 Chuo cha Elimu ya Taifa Kleruu Iringa
· MAFUNZO YA MAKADA WA CCM CHO CHA CCM HURIA: 2004 – 2005
· MAFUNZO YA KAMATI ZA UTENDAJI ZA CCM WILAYA: 1998 Wete Pemba



KAZI NILIZOWAHI KUZIFANYA.
§ Mwalimu wa Shule za Msingi na Sekondari
§ Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya Itikadi na Uenezi
§ Katibu wa UVCCM Wilaya
§ Katibu Msaidizi Mkuu Afisi Kuu ya UVCCM Zanzibar
§ Katibu wa UVCCM Mkoa
§ Katibu wa CCM wilaya

KAZI YA SASA
Katibu Msaidizi Idara ya Itikadi na Uenezi Afisi Kuu ya CCM Zanzibar

UZOEFU WA UONGOZI KATIKA CHAMA NA JUMUIYA
§ Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa ASP Tawi la Shule 1976
§ Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM WA Tawi 1978 – 1983
§ Katibu wa Chipukizi wa Wilaya 1979 – 1983
§ Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya I/Uenezi 1987 – 1992
§ Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Wilaya 1992 – 1996
§ Katibu Msaidizi Mkuu Umoja wa Vijana wa CCM
Afisi Kuu Zanzibar 1996 – 1997
§ Katibu wa Umoja wa Vijana wa CCM Mkoa 1997 – 1998
§ Katibu wa CCM Wilaya 1998 – 2001
§ Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji WAZAZI Wilaya 1984 – 1989
§ Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Vijana
CCM Mkoa 1988 – 1993
§ Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Umoja wa Vijana
wa CCM Taifa 1988 - 1993
§ Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa 1987 – 1992
§ Katibu wa CCM Tawi la Afisi Kuu Zanzibar 2002 – 2007
§ Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 1990
§ Mjumbe wa Kamati ya Usafiri Mapokezi na Malazi
§ ya Maandalizi ya Mkutano Mkuu wa CCM Taifa 2002, 2005na 2006
§ Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya H/Kuu ya Tawi la
§ Kijijini (Umbuji) 2007 – 2012
§ Katibu wa Siasa na Uenezi wa Tawi la CCM Afisi Kuu
Zanzibar 2007 - 2012

Wednesday, July 18, 2007

JEMBE NA NYUNDO SIO MSALABA

JEMBE NA NYUNDO SIO MSALABA

WATANZANIA wa rika yangu yaani wale wote wenye umri wa miaka hamsini na kuendelea waliozaliwa kabla na baada ya kuingia Wakoloni katika nchi mbali mbali Barani Afrika ikiwemo Tanzania, walikuwa mashuhuda wa jinsi wakoloni hao walivyolivamia Bara letu hili na kuwatawala wazee wetu ikiwa ni pamoja na kuwakandamiza, kuwanyanyasa na kuwatesa wananchi wake bila sababu ya msingi. Wakoloni hao walikuja kadhaa za Bara la Ulaya ikiwemo Uingereza, Ujerumani, Ubelgiji, Uholanzi n.k. walimimika kwa wingi Barani Afrika na kugawana mapande ya ardhi ambayo ni Mali halali ya Waafrika na kuanza kuzikalia nchi hizo pamoja na kuwatawala wananchi wake kwa mabavu. Sina haja ya kuelezea kwa upana zaidi juu ya madhila waliyoyapata mababu na wazazi wetu kwa wakati huo, kwani yanaeleweka kwa kila mtu wa Bara hili.

Kuna sababu nyingi zilizochangia kufanyika kwa uvamizi huo. Miongoni mwa sababu hizo ni kwamba wavamizi hao (Wazungu) walijua kuwa Barani Afrika ndilo bara pekee lenye kumiliki mali ghafi nyingi za aina kwa aina ambazo ni pamba, katani, buni, pareto, korosho, mbata, karafuu, n.k. Kama wangezipata bidhaa hizo zingewasidia kwa kiasi kikubwa sio tu kuimarisha viwanda vyao bali pia zingewaletea mapato makubwa zaidi na hivyo kuweza kujitajirisha na kuwa mataifa makubwa kama yalivyo hivi sasa. Waalifanya hivyo kwa vile Waafrika wenyewe walikuwa bado wapo kizani hadi wakafikia mahali wakaliita bara la watu wakizani (bara jeusi). Haya yote yalikuja kutokana na idadi kubwa ya watu wake walikuwa hawahui kusoma na kuandika.

Wahenga walisema “kila penye mbaya wako na mwema wako yupo”. Pamoja na ukweli kuwa wakoloni walikuwa watu wabaya, lakini pia walikuwepo wengine wazuri. Wakijua kuwa watu wanaowatawala hawana elimu kabisa. Wale wenye mioyo mizuri walijaribu kuanzisha shule (skuli) katika badhi ya nchi barani humu na kuwapatia masomo angalau ya kujua kusoma na kuandika. Hali hiyo iliendelea kidogo kidogo hadi kufikia hapa tulipo na kwamba baadhi ya Waafrika waliweza kupata elimu nzuri kiasi cha kujivunia. Aidha, wakiwa na na hivyo kuweza kuelekeza nguvu zaidi katika mapambano dhidi ya wakoloni hao na kadri siku zilivyosonga mbele ndio mapambano yalizidi kupamba moto hadi kufikia Bara zima kuwa huru.

Mapambano ya kutafuta uhuru kwa kila nchi ya Bara la Afrika yalisimamiwa na baadhi ya wana haraka wa nchi husika. Mathalan, aliyeongoza mapambano ya kutafuta uhuru wa nchi iliyokuwa Tanganyika iliyokuwa chini ya Ukoloni wa Kijerumani ni Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Visiwa vya Zanzibar, vilivyotawaliwa na Ukoloni wa Kisultan wa Oman, alikuwa Hayati Mzee Abeid Amani Karume. Watu wengine mashuhuri waliosimama kidete kuhakikisha nchi zao zinakuwa huru ni Jomo Kenyatta (Kenya), Kwame Nkurumah (Ghana), Ahmed Ben Bella (Tunisia), Ahmed Sekouture (Guinea), William Tolbert (Liberia), Kenneth Kaunda (Zambia), Nelson Mandela (SA), n.k. Hao ni baadhi tu lakini kuna wengine kadhaa walioongoza mapambano hayo katika nchi zao hadi kufikia ukombozi kamili.

Mwalimu Julius K. Nyerere, chini ya Chama cha TANU, aliongoza mapambano ya kutafuta uhuru wa Tanganyika kwa muda wa miaka saba (7) – yaani 1954 hadi Disemba 09, 1961, ambapo Tanzanyika ilipopata uhuru. Kwa upande Zanzibar, Hayati Mzee Abeid Amani Karume, chini ya Chama cha Afro Shirazi (ASP), naye kwa muda wa miaka isiyopungua sita (6), aliongoza mapambano dhidi ya ukoloni wa kisultani kuanzia 1957 - Januari 12, 1964, Zanzibar ilipojikomboa katika madhila ya ukoloni na hivyo kuleta faraja kubwa kwa wananchi na hasa wazalendo wa Unguja na Pemba.

Kutokana na busara na hekima za Mzee Karume na Mwalimu Nyerere, kwa niaba ya wananchi wa Zanzibar na Tanganyika, waliweza kuziunganisha nchi hizi mbili hapo Aprili 26, 1964 na kuifanya kuwa nchi moja iliyojulikana kwa jina la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Pamoja na kuungana huko lakini Serikali ziliendelea kubaki mbili ikiwemo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzanai (SMT), iliyoongozwa na Mwalimu J. K. Nyerere na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), chini ya Uongozi wa Mzee Abeid Amani Karume. Aidha, baada ya tukio hilo kubwa la kihistoria, Mzee Abeid A. Karume, alikamata Wadhifa wa Makamo wa Rais wa SMT. Lengo kuu la Muungano huo linaeleweka na kila mmoja wetu nalo sio jengine bali ni kuimarisha zaidi masuala ya ulinzi wa ndani na nje ya mipaka yetu.

Tangu kuasisiwa kwa Muungano huo, Watanzania tumeshuhudia mambo mengi ya maendeleo yaliyosimamia kwa ujasiri na umahiri mkubwa wa viongozi wetu hao. Lakini kuwa na jambo moja la msingi la kujiuliza na kila Mtanzania ? Iweje nchi ya Muungano yenye Rais mmoja iwe na Vyama viwili tofauti ?.

Ilichukua muda wa miaka takriban kumi na mitatu (13), ambapo Watanzania waliposhuhudia Viongozi wao wa Vyama vya TANU na ASP – yaani Mwalimu Julius . K. Nyerere na Mzee Aboud Jumbe Mwinyi (Awamu ya Pili), wakiamua kwa kauli moja na kuviunganisha Vyama hivyo na kuwa Chama Kimoja, Chama chenye nguvu na imara zaidi. Aidha, uunganishaji wa Vyama hivyo kungeweza kujibu suali lililojengeka na kutawala nafsi za Watanzania walio wengi kwamba itawazekanaje nchi yenye Rais mmoja iwe na vyama viwili vyenye itikadi moja ?.

Jibu la suali hili lilipatiwa ufumbuzi Februari 5, 1977, wakati Vyama vya TANU na ASP, vilipoungana na kufanya Chama Kimoja cha Siasa kilichojulikana kwa jina la CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM). Lakini kuzaliwa kwa CCM halikuwa ni tendo la kihistoria tu, bali pia kilikuwa ni kitendo cha kimapinduzi kwa vyama vya TANU na ASP, kukubali kujivunja vyenyewe kwa hiari, heshima na taadhima na kuunda Chama Kipya. Vilifanya hivyo ili kuweza kuendeleza harakati za Ukombozi wa Tanzania. Aidha, kitendo hicho ni uthibitisho tosha wa kukua na kukomaa kifikra, kinadharia, kivitendo na kimuundo kwa TANU na ASP. Kwa mantiki hiyo, wazo la kuunganisha vyama hivyo halikuwa jambo jipya kwa ASP na TANU. Mathalan, ASP ni matokeo ya Muungano baina ya ‘African Association’ na ‘Shirazi Association’.

Hivyo, kuzaliwa kwa CCM ni kitendo dhahiri cha kutekeleza Katiba ya Muda ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1965 iliyosema “Kutakuwepo Chama Kimoja cha Siasa katika Tanzania …. Mpaka Vitakapoungana Chama cha TANU na ASP (ambavyo vikiungana vitaunda Chama Kimoja cha Siasa), lakini kwa sasa Chama cha Tanganyika kitakuwa TANU na Zanzibar kitakuwa Chama cha ASP”.

“Mwenye macho haambiwi tazama”. Kila Mtanzania amejionea mwenyewe jinsi CCM ilivyopania kuondoa kero mbali mbali zilizoikumba jamii ya Tanzania na kuleta maendeleo endelevu nchini humu kwa maslahi ya jamii nzima. Miongoni mwa mambo yaliyopatika ni pamoja na kuimarishwa kwa Mmiundombinu ya Kiuchumi na Ustawi wa Jamii, Mawasiliano, Afya, Elimu, n.k. Kama hiyo haitoshi, CCM imeweza kufanikisha azma yake ya kudumisha amani na utulivu wa Taifa letu.

Jambo la kushangaza na kwa kweli linasumbua kwa kiasi kikubwa nafsi za Watanzania walio wengi ni ile kauli ya kupotosha inayotolewa na kusambazwa na baadhi ya Watanzania kwamba “CCM SIO CHAMA CHA WANANCHI WA TANZANIA NA KWAMBA NEMBO YA JEMBE NA NYUNDO ILIYOMO KWENYE BENDERA YAKE NI ALAMA YA MSALABA”. Hakika, kauli hiyo na nyengine kama hizo ni za kupotosha.

Wednesday, July 11, 2007

WAPINZANI KUSHINWA KABLA YA UCHAGUZI

Wapinzani wameshindwa hata kabla ya uchaguzi

Wakati tunakaribia katika Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar imebainika wazi kwamba hofu imewakumba wapinzani na hasa Chama cha Wananchi (CUF) kiasi cha viongozi wao kuashiria kushindwa kabla ya uchaguzi wenyewe kufanyika.

Dalili za kushindwa zianza zamani, pengine kabla ya kuanza kamapeni. Hofu hiyo iliibuka mara ya baada ya Rais wa Zanzibar, Abeid Amani Karume kutangazwa kugembea tena nafasi hiyo ya Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi m(CCM).

Kabla ya mchakato wa kumpata mgombea huyo, wapinzani walikuwa wakifanya vibweka vingi huku wakijigamba kuwa wataing’oa CCM katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 30, mwaka huu.

Matumaini makubwa waliyokuwa nayo CUF ya kuishinda CCM yalitokana na mawazo yaliyokuwepo kwamba kuna utofahamiana miongoni mwa viongozi wa CCM na hivyo kuweka tama ya fisi ya kutegemea kudongoka mkono wa binadamu.

Kimsingi, mawazo hayo yaliyobeba hisia za propaganda chafu yalikuwa na malengo ya kutaka kuwahadaa wafuasi wa CCM na kuwachanganya viongozi wao kabla ya kuanza mchakato wake wa kumpata nahodha atakayeipeperusha bendera yake katika kinyang’anyiro cha urais.

Katika kuiangalia propaganda hiyo, imebainika dhahiri kwamba ilitokana na woga, hofu na waswasi wa kuangushwa vibaya katika kinyang’anyiro hicho,
Baada ya wapinzani kutofanikiwa hila zao za kuingiza mamluki katika uandikishaji wa Daftari la Kudumu la wapiga kura.

Si hivyo tu, lakini CUF katika kujitafutia uhalali wa kuwa chama pekee chenye upinzani wenye nguvu Zanzibar, kilijaribu sana kutaka kuvizuia vyama vingine vya upinzani visiweke wagomea katika nafasi ya Urais wa Zanzibar.

Mbinu hiyo ilikuwa ni kutaka kuhakikisha kwamba wafuasi wote wa upinzani wanampigia kura mgombea wa CUF katika nafasi hiyo ya Urais wa Zanzibar.

Hilo halikuwezekana kwani vyama vitano vimejitokeza kuweka wagombea wao. Vyama hivyo ni CCM, CUF, Jahazi asilia, UDP na

Kutokana na hali hiyo, inajitokeza wazi kwamba uchaguzi wa mwaka huu, mambo yatakuwa mambo kweli kwani takriban vyama vyote vilivyosimamisha wagombea wao vimeadhimia kushiriki kikamilifu katika uchaguzi huo na sio kuibeba CUF ambayo hivi sasa inahitaji kupatiwa msaada wa damu kutoka kwa vyama hivyo.

DALILI ZA KUSHINDWA
Wakati wakujifaragua kwamba mwaka huu lazima CUF ipate ridhaa ya wananchi kuongoza dola, majinato yao yamekoma baada ya hila zao nyingi kushindwa.

Hila za CUF zilianza kukwama tokea wakati wa uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura ulipoanza kisiwani Unguja. Kilichoandaliwa na chama hicho katika uandikishaji huo ni kupandikiza watu wasio na sifa za ukaazi.

Kwa kutumia wafuasi wa chama hicho wanaoishi katika mikoa ya Tanzania Bara, Kenya na nchi za Ghuba, CUF ilijipanga kuandiokisha wapiga kura wengi. Mbinu hiyo iligunduliwa na CCM kwa kutotoa mwanya wa kuandikishwa wasiohusika kwenye daftari hilo la wapiga kura.

Kushindwa kwa mbinu hiyo kuliishia kwa chama hicho kutoa malalamiko yaliyodai kutoandikishwa wafuasi wao wapatao 10,000. Malalamiko hayo yalikuwa ni kuashiria kukubali kushindwa.

Kwa kufahamu kwamba idadi ya walioandikishwa kwenye daftari la wapiga kura haiwezi kukipatia CUF ushindi katika Uchaguzi Mkuu, hila ya kutaka kulichafua daftari hilo zilionekana kushamiri. Kwa kuitumia kampuni ya Waymark kulijitokeza ishara za wazi za kiharamia zilizofanya na kampuni hiyo.

Miongoni mwa uharamia uliofanywa na kampuni hiyo ni kuibwa majina ya wapiga kura 30,000 baada ya kampuni hiyo kuruhusiwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar kuhakiki kwa majaribio majina ya wapiga kura 10,000.

Aidha, mipango ilikuwa inafanywa na kulisafirisha nje ya nchi daftari la wapiga kura kwa kisingizio cha kwenda kulihakiki ili kubaini majina ya wapiga kura wanaofaa na wasiofaa. Kitendo hicho kilikuwa ni cha kutiliwa mashaka makubwa hasa baada ya kubainika wizi uliokwishafanyika wa majina 30,000 ya wapiga kura.

CCM ilitegua mtego huo uliowekwa ambao ulikuwa na mkakati maalumu wa kuharibu daftari hiyo kwa maslahi ya kuwapendelea wapinzani. Kugunduliwa kwa mtego huo pia kulipelekea CUF kulalamika kiasi cha kutishia kugomea kushiriki kwenye uchaguzi wenyewe iwapo hakukufanyika uhakiki. Malalamiko hayo pia yanaashiria kukubali kushindwa.

Kipigo walichokipata wapinzani kilichotokana na utambulisho wa kishindo ulioambatana na umati wa wananchi waliojitokeza kumuunga mkono mgombea huyo wa CCM, Abeid Amani Karume alipokwenda Tume ya Uchaguzi kuchukua fomu za kugombea Urais kilitosha kubainisha kukubalika kwake kwa umma.

Umati huo wa watu ulitoa taswira kamili ya CUF kushindwa kwani pamoja na wapinzani kwa muda mrefu kujilabu kwamba wanaungwa mkono na wananchi wengi, siku hiyo ilionekana wazi kuwa mawazo hayo yaliyokuwa ni kinyume chake.

Katika harakati za kutambulishwa wagombea wa CCM baada ya kuteuliwa na chama chao viongozi wa kitaifa wa CUF walikuwa wa kwanza kutangaza kulalamikia utambulisho huo. Madai waliyoyatoa ni kuwa CCM imeanza kampeni kabla ya wakati huku viongozi hao wa upinzani wakisahau mikutano waliyokuwa wakiifanya katika kuwahamasisha wafuasi wao kujiandaa mithili ya wanasuburi kwenda vitani.

Viongozi hao wa CUF pamoja na kulalamika kuwa CCM imeanza kampeni kabla ya wakati, walikuwa wakitishwa na wimbi la wafuasi wake wakiwemo viongozi waandamizi na Wabunge wa chama hicho kujitoa na kujiunga na CCM. Matukio hayo ni dalili tosha zinazoashiria kushindwa kwa chama hicho.




Mbali na hali hiyo CUF, tayari imeshalalamika kuwa uchaguzi huenda usiwe huru na wa haki kwa sababu ya kutokuwa na imani na mchakato mzima wa kuandikisha wapiga kura.

Tamko la Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Sharif Hamad la kubainisha kwamba hatokubali mmatokeo yoyote ya uchaguzi hata endapo yeye mwenyewe atashinda lilitosha kubainisha kulia uteka. Matamshi hayo ni sehemu ya kukata tama kabla ya hata uchaguzi haujafanyika.

Vigezo vyote hivyo vinaweka bayana kushindwa kwa CUF katika Uchaguzi Mkuu wa Zanzibar utakaofanyika Oktoba 30, 2005. Hali hiyo sasa inafahamika hata kwa baadhi ya wafuasi wa chama hicho na ndiyo iliyoshusha hamasa za wafuasi hao za kwenda kwa wingi katika mikutano ya hadhara imepungua sana hivi sasa ikilinganishwa na hali ilivyokuwa kabla.

CUF iliyozoea kushindwa na badala yake kudai kuwa wameibiwa kura kama ilivyofanya mwaka 1995 na 2000, tayari imeshaonesha dalili za kushindwa tena mara ya tatu mfululizo ambapo viongozi wa chama hicho wanaeleza wazo kuwa kuwa huenda mambo yakawa kama yalivyokuwa chaguzi ziliopita.

Kwa kufahamu hivyo, ndio maana chama hicho kikatoa tamko la kutaka kususia uchaguzi Zanizbar iwapo madai kilichotoa juu ya hitilafu kwenye daftari la kudumu la wapiga kura hazitapatiwa ufumbuzi kwa muda maalumu uliotolewa ambao umeshamalizika.

Kinachodhihirika ni kubainika wazi kwamba upinzani umeshashindwa hata kabla ya kupigwa kura. Na kinachoshindilia msumari wa mwisho katika jeneza hilo la CUF ni kujitokeza kwa wingi wafuasi wa CCM kwenye mikutano ya kampeni ya CCM. Wingi huo unaifanya CCM kuendelea kuzoa kura katika uchaguzi ujao na dalili tosha ya ushindi wa kishindo.

VOTI KWA CCM

VOTI KWA CCM


Kwanza kabisa sina budi kumshukuru Mwenye Munngu Mtukufu kwa kutujaalia uzima na afya njema na pia kutupa uwezo wa kutekeleza sunna muhimu ya Funga iliyokokotezwa na Mola Karima ya Mwezi huu Mtukufu wa Ramadhan, kwa wale Waumini wa Dini ya Kiislam.

Ndugu wana CCM na wananchi kwa ujumla, kama mjuavyo, kesho ni siku ya Jumapili tarehe 30 Oktoba, 2005. Ni siku muhimu sana katika historia ya Taifa letu la Tanzania Zanzibar. Ni siku iliyopangwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu, kwa lengo la kuwachagua viongozi mbali mbali wa kitaifa ikiwa ni pamoja na Rais wa Zanzibar, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani.

Chama cha Mapinduzi kinaamini kwamba wananchi walio wengi wa Unguja na Pemba, wanauelewa mkubwa hususan masula ya kisiasa na kwamba watakuwa tayari kuitumia kikamilifu haki zao za kikatiba na kidemokrasia, jambo ambalo linatoa faraja kubwa sana kwa CCM. Kwa kuzingatia hali hiyo, sina budi kuwanasihi wana CCM na wananchi wapenda amani na utulivu wote kujitokeza kwa wingi siku hiyo na kwenda vituoni Mijini na Vijijini kwa dhamira moja tu nayo sio nyengine bali kwa ajili ya kupiga kura. Kufanya hivyo mtakuwa tayari mmetekeleza vyema haki yenu hiyo ya kuchagua viongozi mnaowataka katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu wa 2005.

Chama cha Mapinduzi kinawataka kuwatoa wasiwasi wananchi wa visiwa vya Unguja na Pemba kuwa kuna njama na hila zilizopangwa na baadhi ya vyama vya upinzani vyenye lengo la kutaka sio tu kuwatisha wananchi na hasa wana CCM ili washindwe kwenda vituoni kupiga kura zao bali pia wanakusudia kuvuruga Uchaguzi huo na hivyo usifanyika kama ilivyokusudiwa.

Kwa niaba ya Chama cha Mapinduzi nachukua fursa hii kuwahakikishia wana CCM na wananchi wapenda amani wote wa Taifa hili kwamba ulinzi umeimarishwa mara dufu na hivyo hakuna mtu au kikundi cha watu kitakachopata nafasi ya kutisha watu mitaani katika siku hiyo tu ya upigaji kura bali hata baada ya shughuli hiyo nzito kukamilika. Kikubwa zaidi ni kujitokeza mapema katika vituo mlivyopangiwa na kufanya shughuli hiyo muhimu na kuwachagua viongozi mnaowataka na hasa wagombea wote wa CCM ili waweze kuendelea kuwaleta maendeleo endelevu kwa maslahi yenu na vizazi vyenu vya leo na vijavyo bila ya ubaguzi wa aina yoyote.

Kwa kuwa haki ya kupiga kura ni ya kila raia aliyetimiza umri na masharti yaliyowekwa na Tume ya Uchaguzi, Chama chetu cha Mapinduzi, kitaendelea na juhudi zake ikiwa ni pamoja na kuvitaka vyombo vya dola kuimarisha zaidi ulinzi ili kila raia na hasa kila mzalendo mwenye haki ya kupiga kura aweze kuitumia vyema haki yake hiyo. Hivyo, ndugu wana CCM na wananchi msikubali kubabaishwa kwa kauli za uzushi zinazotolewa na watu mitaani kwani hali ya ulinzi imeimarishwa kwa kiwango cha hali ya juu mno. Jambo la msingi ni kuamka asubuhi mapema, nenda kituoni, jipange kwenye mstari, piga kura yako kwa kuwachagua wagombea wote wa CCM kuanzia Mgombea wa Kiti cha Urais wa Zanzibar, Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani. Ukimaliza kufanya hivyo rejea nyumbani kusubiri matokeo yatakapotangazwa na Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar na hatimaye ushangilie ushindi.

Kwa nini tunasema hivyo? Tunasema hivyo kwa sababu Chama cha Mapinduzi ndio Chama pekee chenye wanachama na wapenzi wengi zaidi kuliko Chama chengine chochote cha siasa hapa nchini. Aidha ni Chama pekee chenye nia thabiti ya kuwaletea wananchi maendeleo endelevu kutokana na Sera zake zinazotekelezeka siku hadi siku. Sote ni mashuhuda wa jinsi gani Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, chini ya Uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Amani Abeid Karume, alivyofanikiwa kusambaza kwa kiwango cha hali ya juu mno ikiwa ni Utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2000. Sina haja ya kuyataja yote yaliyopatikana. Miongoni mwake ni pamoja na :-

· Uchumi wa Taifa umekua kwa asilimia sita nukta tano (6.5%) pamoja na kusimamia vyema matumizi ya mapato.
· Miundo mbinu
Barabara mpya kwa kiwango cha lami zimejengwa Unguja na Pemba.
· Vituo vya Afya vimejengwa Mijini na Vijijini
· Umeme – umesambazwa karibu nchi nzima
· Maji safi na salama yanapatikana Mijini na Vijijini
· Serikali imefanikiwa kujenga mazingira mazuri ya uwekezaji
· Sekta ya Elimu
i) Skuli zimeenea na mabanda yameongezeka mara dufu
ii) Vyuo Vikuu hadi kufikia vitatu
· Mawasiliano na Uchukuzi
i) Makampuni ya Simu za mkononi kama vile Zantel, Vodacom, Mobitel, Celtel n.k. zimeanzishwa na kuendelea vizuri.
ii) Usafiri wa Anga na baharini vimeimarishwa
iii) Viwanja vya ndege vya Unguja na Pemba vimepanuliwa n.k.

Kwa mantiki hiyo, wapinzani hawana uwezo wa kuishinda CCM katika Uchaguzi Mkuu huu, kwa sababu hawana Demokrasia ya kweli ndani ya vyama vyao. Hivyo, natumia fursa hii kuwaomba wana CCM na wananchi wapenda amani wote kwenda kwenye vituo vya kupigia kura kwa salama na amani. Baada ya kukamilisha kupiga kura yako, ondoka na urejee nyumbani bila ya tatizo lolote. Aidha, Chama cha Mapinduzi kinawaomba wana CCM wote kutovaa sare za Chama chetu. Hili sio ombi bali ni amri, kwani kuvaa sare kwa siku ya kupiga kura ni kosa la jinai.

UJIO WA WAANGALIZI WA KITAIFA NA KIMATAIFA:
Chama cha Mapinduzi kimefarajika na hali ya ujio wa Waangalizi wa Uchaguzi kutoka Jumuiya ya Madola waliofika nchini kwa lengo la kuja kuangalia jinsi Uchaguzi huu utakavyofanyika. Aidha, nachukua nafasi hii kuwashukuru kwa kumiminika kwa wingi. Lakini CCM inasema kwa kuja nchini humu kwa lengo la kuja kushuhudia jinsi gani Uchaguzi unavyofanyika na sio wamekuja kutoa maelekezo ya jinsi gani Uchaguzi huu ufanyike wala kutoa matokeo ya Uchaguzi huo.

Chama Cha Mapinduzi kinaamini kuwa kuwepo kwao kutasaidia kwa kiasi kikubwa kufikisha taarifa sahihi kwenye Jumuiya ya Kimataifa kuhusiana na hali halisi ilivyo kuanzia uwingi wa wanachama na hata wapenzi na pia jinsi gani walivyohamasika na kuwa tayari wakisubiri siku yenyewe kufika ili waweze kutumia haki zao za kidemokrasia na kuchagua viongozi wanaowataka bila ya wasiwasi wowote. Aidha, kuwepo kwao kutasaidia kubainisha ukweli na uongo wa viongozi wa vyama vya upinzani wanaojaribu kuihadaa dunia eti CCM haina wanachama na pia hawapendwi na jamii ya Wazanzibari. Kupitia mkutano wa Ufungaji wa Kampeni za CCM uliofanyika leo, tunaimani kubwa kwamba Waangalizi wameweza kujionea wenyewe hali halisi na hivyo kuweza kupima na kutambua ukweli na uongo wa vyama hivyo vya upinzani nchini.

Mwisho, kwa mara nyengine tena nachukua fursa hii kuwataka wana CCM na wananchi wapenda amani na utulivu wote wa Taifa letu, kujitokeza kwa wingi kwenye vituo vya kupigia kura ili kwenda kupiga kura zenu na kukipatia ushindi wa nguvu ya tsunami Chama chenu cha Mapinduzi na hivyo kukipa ridhaa kwa mara nyengine tena ya kuongoza dola kwa miaka mingine mitano ijayo.

Ahsanteni.
KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI.


(VUAI ALI VUAI)
KATIBU – IDARA YA ITIKADI NA UENEZI
CHAMA CHA MAPINDUZI
ZANZIBAR.

Monday, July 9, 2007

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) kimewataka wanachama na wafuasi wake kutobabaika na kauli zilizotolewa na CUF za kudai kwamba kuna vijana wengi wa CCM wamejiunga na chama hicho cha upinzani.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari leo na Katibu wa Idara ya Itikadi na Uenezi wa CCM Zanzibar, Bwana Vuai Ali Vuai, +imeeleza kuwa kauli hizo ni za uongo na hakuna mwanachama yeyote aliyehama CCM na kujiunga CUF.

Bwana Vuai ameeleza kuwa baada ya kufuatilia kauli hiyo katika maeneo yaliyoelezwa kwamba kuna vijana waliojiunga na chama hicho, CCM imebaini kuwa taarifa hizo zilikuwa hazina ukweli.

Ameeleza kwamba kutokana na kufuatilia huko imefahamika vijana waliotangazwa kutoka CCM ni miongoni mwa vijana wa chama hicho cha upinzani wa maeneo ya Shangani huko Mkokotoni ambao walipangwa kurejesha kadi za kughushi ambazo hazikuwa kadi halali za CCM.

Amewataka wananchi kutobabaishwa na propaganda za uongo ambazo ni mfululizo wa kauli za upotoshwaji zinazotolewa na viongozi wa CUF kwa vipindi chote hata kabla ya kuanza kwa mikutano ya kampeni.

Bwana Vuai alisema viongozi wa upinzani wamekuwa wakifanya hivyo kwa kufahamu kwamba CCM itaendelea kushinda katika uchaguzi ujao Tanzania Bara na Zanzibar kutokana na kukubalika kwake mbele ya jamii.

Alifahamisha kuwa ushahidi wa CCM kuendelea kuongoza nchi unabainika kutokana na chama hicho kushinda viti 200 kabla ya hata uchaguzi vikiwemo viti vinane (8) vya ubunge na 192 udiwani.

Alieleza kuwa hicho ni kigezo tosha cha kuthibitisha kwamba wananchi wameridhika na utekelezaji wa ilani za CCM za mwaka 2000 ilisababisha kuimarika kwa miundo mbinu ya kiuchumi na ustawi wa jamii nchini.

Hivyo, Bwana Vuai ameitaka CUF kuacha mara moja kutoa kauli za kubabaisha kwani kufanya hivyo ni kuzidi kuidhihirishia dunia kuwa tayari kimekata tamaa ya kupata ushindi kwa chama hicho katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 30, mwaka huu.

KIDUMU CHAMA CHA MAPINDUZI


………………
(Vuai Ali Vuai)
Katibu – Idara ya Itikadi na Uenezi
Chama cha Mapinduzi
ZANZIBAR

20/10/2005
Ndugu Mhariri

Naomba nafasi ili niweze kutoa maoni yangu juu ya bei ya mafuta iliyopo hapa nchini.

Ni muda mrefu sasa tokea Bodi ya Mapato nchini kupitia Afisa wake wa kodi kututangazia Wazanzibari kuwa Serikali imejitoa katika kudhibiti bei za mafuta nchini ili wafanyabiashara wa bidhaa hiyo wapange bei kwa mujibu wa gharama halisi za biashara hiyo.

Kutokana na ufahamu wangu mdogo wa biashara nilitegemea kuwa bei ya mafuta nchini hivi sasa ingepungua kama ilivyo nchi nyingi duniani kutokana nakuongezeka uzalishaji hasa nchi zenye kuzalisha kwa wingi mafuta (OPEC). Vile vile, kwa upande wa shilingi ya Tanzania nayo imeimarika kidogo siku hizi thamani yake kuliko kipindi ambacho bei ya mafuta ilipanda hadi kufikia bei Tshs. 1350, kwa Petroli na 1320 kwa Disel. Kipindi hicho dola moja ya Kimarekani ilikuwa niTshs. 1320 kuinunua. Hivi sasa dola moja ya Kimarekani ni Tshs. 1275 kuinunua. Wakati huo huo, Pipa moja la mafuta hapo kabla katika Soko la Kimataifa likiuzwa dola 79 na hivi sasa ni dola 62.

Kwa hiyo,kutokana na mwenendo huo wa bei, kimataifa ilitakiwa bei ya mafuta nchini nayo ipungue hasa kutokana na Serikali kujitoa katika kuhodhi bei ya mafuta nchini na kwa uchache bei iwe kama ilivyo Tanzania Bara ambapo bei hivi sasa kwa lita moja ya Petroli haizidi 1270 hata kwa Mikoa iliyoko mbali na Bandari ya Dar es salaam.

Mwisho ningeiomba Wizara au Idara inayoshughulikia mwenendo mzima wa bei za bidhaa na huduma nchini kufuatilia kwa karibu zaidi bei zinazopangwa na wafanya biashara ambao hawajali maisha ya wananchi wa kawaida bali wanajali faida yao ili mpango wa kupunguza umasikini ufanikiwe nchini kwani kupanda kwa bei holela kwa bidhaa muhimu au kutopungua bei zake hata kama masoko mengine yamepunguza bei zake ni kutomtendea haki raia wa kawaida anaebebeshwa mzigo huo kwa njia isiyo ya moja kwa moja na maana halisi ya kuwepo soko huria itakuwa haina maana. Ni tegemeo langu kwamba Serikali nayo itaingilia kati suala hili pale inapoona kuna wakorofi wachache wanaoweka tamaa mbele kibiashara kuliko urahisia wake.


‘MWANANCHI MPENDA MAENDELEO’


………….
ALI SAID MUSSA
MAGOMENI
ZANZIBAR

JKAMPENI ZA UCHAGUZI MWEZI WA RAMADHANI

Ndugu Mhariri,

Napenda kuomba nafasi kupitia gazeti lako kutoa maoni yangu kuhusiana na mwenendo wa Uchaguzi unaoenedelea hivi sasa nchini tukiwa kwenye kipindi cha Kampeni.

Kwanza sina budi kutoa pongezi zangu kwa Chama Cha Mapinduzi kwa utaratibu wake wa kufanya mikutano ya Kampeni wakati wa asubuhi ili wanachama wake wapate nafasi ya kujitafutia riziki na kufanya Ibada katika kipindi hichi cha Ramadhani sote ni welewa wa mambo kuwa fadhila za mwezi wa Ramadhani kwa wanaofanya Ibada ni kubwa sana kuliko miezi mengine yoyote ya Kiislamu. Aidha Waisalamu wanatakiwa wawe waaminifu, wakweli na waungwana na kuepukana na kauli ambazo zitawafanya wasitafautiane na wale wasiofunga katika kipindi hichi. Vile vile yale yaliyomo kwenye dhamira zao yafuatane na vitendo vyao.

Nimeamua kutumia neno dhamira kwa kuwa ndio inayomuhukumu mtu hata kama jambo hajalifanya ila anakusudia kulifanya kwani tunaambiwa kwenye hadithi za Mtume kuwa “Hakika vitendo vinafuatana na nia na kila mtu atalipwa kutokana na nia yake” Kutokana na kukaribia Uchaguzi Mkuu na huku baadhi ya vyama tayari vishakata tamaa ya ushindi licha ya kutamka kuwa vitashinda hadharani ili kuwapa moyo wafuasi wake na kuwalaghai kwa ajili ya lengo lao waliloliweka na hasa baada ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika tarehe 30/10/2005. Nimeamua kusema kuwa baadhi ya vyama vya Siasa vimekata tama ni kutokana na ushahidi nilionao wa watu hao kutumia mikutano ya siri na kututaka tujitayarishe kwa maandamano makubwa baada ya Uchaguzi ya kudai kupokonywa ushindi kinachonishangaza na kinachonifanya kuamua kuandika barua hii ni kutaka kuwatahadharisha wananchi wenzangu kuwa suala la kunyanganywa ushindi kwa atakaeshinda halitowezekana hata kidogo kutokana na taratibu nzuri zilizoandaliwa za kuhesabu kura na kutangaza matokeo kwa jumla ambapo vyama vyote vinatakiwa kuweka Mawakala bila ya shaka sote ni mashuhuda wa kauli za viongozi wakuu wote wa Vyama na hasa Chama Cha CUF ambao wamekiri wenyewe kuwa utaratibu ulioandaliwa na Tume ya Uchaguzi utapelekea kufanyika kwa Uchaguzi huru na wa haki. Sasa kinachonishangaza na kunifanya nikumbuke swaltul-Munafiqina ambayo imewaeleza kwa urefu na mapana watu ambao dhamira zao siku zote haziendeda na kauli zao ni kutaka kujua hayo maandamano wanayotaka kufanya ni kwa ajili ya nini na maslahi ya nani ikiwa tayari tumejenga uaminifu kwa Tume na tumekubali kuyapokea matokeo ya kura na haya ya Urais. Hivi viongozi wa CUF wanapotutaka siku watakayotutangazia kwa siri maandamano waliyoyatayarisha na kututaka tushiriki na kuwatanguliza wazee mbele kwa kile wanachokidai kuwa wakifa wao si hasara kwa kuwa washaonja chumvi nyingi na baadae wafuatie vijana na mwisho wanawake. Hivi ni kweli hawa viongzoi wa CUF wanaitakiwa mema nchi yetu na sisi wananchi?.

Jambo ninalotaka kuwaambia viongozi wa CUF ni kuwa wananchi wengi hivi sasa si wajinga na wanathamini uhai wao na wanafahamu kuwa mfa maji hukamata maji, kwa hiyo wasiwe na tamaa ya kutufanya chambo kwa kuwa tu bwana mmoja kakosa Urais. Hayo maandamano yake atakayoyafanya atayafanya yeye na Bwana Said wake ambao wamekula kiapo cha kufa kwa ajili yake na wale waliokata tamaa ya maisha lakini wengi tumechoka na ule wimbo wetu wa akikosa Seif tumekosa sote. Tukumbuke kuwa kupata au kukosa yote ni Majaaliwa. Na Mola amesema kuwa humpa Ufalme amtakae na humnyima amtakae. Hivi Maalim Seif akikosa yeye ndio atake sisi atufanye kuku wa muhanga? Kwa hilo tunamwambia hawai na tunamtakia kila la kheri katika maandamano atakayoyaongoza na kuzungukwa na hao wakubwa wake. Mwisho nawataka viongozi wa CUF wasome Shishtul Munafinna na hasa aya ya nane ya sura hiyo mwisho kabisa nawataka wana CUF wajue kuwa akishindwa Seif safari hii tisichoke kwani 2010 haiko mbali panapo uhai tumpe tena nafasi kwani kuvunjika kwa koko sio mwisho wa utunzi. La muhimu kwetu ni “AMANI” kwani hiyo ndio siri ya mafanikio na maendeleo na sio “UPANGA” utakaotupeleka kwenye hilaki. Mola tunakuomba utudumishie AMANI yetu dhidi ya Mahasidi wa nchi yetu. AMIN


RAIA MWEMA
ZANZIBAR