Monday, July 9, 2007

DEMOKRASIA NINI!

DEMOKRASIA inamaana pana sana katika uwanja wa siasa. Asili ya neno Demokrasia linatokana na lugha ya Kiyunani (Kigiriki) ambalo msingi wake ni maneno mawili DEMO ambalo maana maanayake watu na KRATOS likiwa namaana ya uyo mtutawala. Kwa kifupi maana ya neno ni Utawala wa Watu, kwa kumaanisha matakwa ya watu wengi. Na kinyume chake ni Autokrasi ya Udikteta. Kwa ufupi Demokrasia maana yake ni wengi wape au kukubali na kuheshimu maamuzi ya wengi. Kwa maana hiyo mtu hawezi kuwa mwanasiasa, bila kuwa mwanademokrasia, lakini inawezekana kuwa mwanademokrasia pasi na kuwa mwanasiasa. Kwa kuwa demokrasia ndio msingi mkubwa wa siasa, hivyo mwanademokrasia anaweza kuwa mwanasiasa mzuri kwa sababu ana msingi madhubuti wa kuelekea kuwa mwanasiasa.

Hata hivyo, mtu anaweza akawa na sifa zote hizo mbili na pia inawezekana akawa hana sifa hata moja katika hizo, lakini akajipa sifa hizo kwa nguvu. Kwa kukamilika, mwanasiasa mzuri lazima awe pia mwanademokrasia.Mwanasiasa mzuri lazima awe mtu mtaratibu, mpole, mstaarabu na mwenye kushauriana na wenziwe na awe anakubali kukosolewa. Kubwa zaidi awe mwenye subira na mstahamilivu, kupungukiwa na sifa hizo, ni kukosa muhimili wa kuwa mwanasiasa.

Mwanasiasa siku zote huwa mkweli na muaminifu anayoyasema hayatofautiani na anayoyatenda Kwasababu hao waliojipachika uwanasiasa maneno yao tafauti kabisa na vitendo vyao, basi hatuwezi kuwaita wanasiasa bali ni wababaishaji tu wa siasa.

Nchini Tanzania tangu uanze mfumo wa vyama vingi, mwaka 1992 karibu kila mtu anajifanya mwanasiasa na wengine kudiriki kuunda vyama. Kwa kuangalia nyendo za watu hao inaonekana wanapenda kuwa wanasiasa bila ya kuwa na misingi ya uwanasiasa, hivyo wanashindwa hata kukaribia kufikia hadhi hiyo.

Katika kufuatilia kwa karibu nyenendo za baadhi ya wanasiasa, imebainika baadhi yao huwa wanatafuta kura za wananchi ili ziwawezeshe kutimiza matakwa yao ya kajipatia umaarufu, maslahi binafsi na katambulika ili waweze kupatamadaraka.

Kigezo nakipimo kikubwa cha kumfahamu mwanasiasa, kiko katika kuangalia nyendo zake na kuzilinganisha na misingi ya demokrasia. Misingi hiyo inazingatia Uhuru na Haki, kupinga aina zote za ubaguzi, ama wa rangi, kabila, dini, jinsia au umajimbo na kutoa haki yakila mtu kushiriki katika mambo ya utawalawa nchi. Jambo la muhimu katika misingi hiyo ni nidhamu, inayolazimisha wacheche wakubaliane na matakwa ya wengi,kila mtu awe na haki kuchagua au kuchaguliwa kuwa kiongozi.

Kwa mtazamo huo demokrasia inaweza kuwapa mahali popote ndani ya mfumo wa vyama vingi vya siasa au katika mfumo wa chama kimoja mradi tu, misingi hiyo mikubwa inafuatwa. Hivyo demokrasia nchini Tanzania ilianza tangu enzi ya mfumo wa chama kimoja.

Zanzibar imeshuhudia awamu tofauti za uongozi. Pamoja na yote hayo kumekuwa na baadhi ya watu wanadai ukombozi wanchi. Swali liliopo ni nani anayetawala Zanzibar! Jibu lake linaweza kuwa na utata, kwani litahusishwa moja kwa moja na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar imemezwa na Tanzania Bara. Kutakana na majibu ya aina hiyo ndipo hoja ya kusema kwamba kuna watu wanaojiita wasiasa, inapopata nguvu, kwani mwelekeo wa watu hao sio kujenga Taifa lenye nguvu, bali ni kudhofisha na kuleta mgawanyiko miongoni mwa jamii. wa Zanzibar katika kipindi hiki, wanataka kuikomboa Zanzibar kutoka katika mikono ya nani! Zanzibar hivi sasa inatawaliwa na wananchi wenyewe, wanyonge, wavuja jasho, wakwezi na wakulima. Anayetaka kuondoshwa madarakani ni nani! Na nani awekwe badala yake.

Nadharia hiyo ya kudai ukombozi ndani ya Taifa huru iliibuka katika kipindi kirefu ndani ya mfumo wa chama kimoja cha siasa. ASP na baadae mwaka 1977 CCM Mjaribio kadhaa yasiofaulu ya kutaka kuipindua Serikali ya Zanzibar yaligundulika moja kati ya hilo ni lile lililopelekea kuuwawa kwa Rais wa kwanza wa Zanzibar Mzee Abeid Amani Karume, Aprili 7, 1972. Mjumuiko wa matukio hayo, ni ishara iliyowazi kwamba athari za siasa za vyama vilivyokuwepo kabla ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964 ziliendelea kubaki licha ya vyama hivyo vilivyokuwa vikipigania uhuru kuvunjwa baada ya Mapinduzi hayo. Hivyo wafuasi pamoja na baadhi ya vizazi vyao walikuwa wakiendesha sera za vyama hivyo za kugombania ukombozi.

Kikwazo kikubwa kilichosiisha kutimiza kwa azma hiyo ya wafuasi wa vyama vya kale ni Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambao kwa muundo wake, siojambo linalowezekana kuipindua Serikali ya Zanzibar pekeyeke bila ya kuihusisha Serikali ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jumla. Hivyo jmabo linalohitajika kufikisha lengo hilo ni kuparaganya muungano huo ambapo hila na mbinu mbali mbali za kuuvunja zilipangwa na kutekelezwa kufanikiwa.

Kuja kwa mfumo a vyama vingi nchini 1992 na kuanzishwa kwa chama cha upinzani Zanzibar hasa Chama Cha Wananchi (CUF), kuliipa nguvu mpya mikakati hiyo kwani mbinu zilizotumika katika kukisimamisha chama hicho, zilikuwa hazina tofauti na zile zizotumwa kuvisimamisha vyama vya zamani ZNP na ZPPP na hasa Pemba. Wananchi walishurutishwa kujiunga na chama hicho, na walionekaniwa kutounga mkono CUF,walitengwa, walisuswa kununuliwa bidhaa zao, waligomewa kuuziwa bidhaa kwenye maduka na masoko,walitengwa kwenye shughuli za kijamii kama vile misikitini, mazikoni maharusini makazini nk,walinyimwa hata maji ya kunywa visimani. Pamoja na shinikizo zote hizo wapo waliokataa kuiunga CUF, hao hao walifanyiwa vitendo vya kinyama kabisa, waling’olewa mazao yao katika mashamba, walihamishwa kwa nguvu katika mitaa, wanaume waliachishwa wake zao na kwa wanawake waliachwa na waume zao, na wengine kufika hata kupakiwa kinyesi cha binaadamu kwenye milango na
madirisha ya nyumba zao.

Harakati hizo zilianzishwa na kundi maalum ambalo hapana shaka lina malengo iliyo kusudia.Mipango hiyo inaweza kuhusishwa naile iliyokuwepo wakati wa kugombania uhuru. Lakini katika kufahamu kwa uwazi chimbuko la yote hayo, ipo haja ya kufahamu mwenendo wa muelekeo wa kiongozi mkuu wa kundi hilo kuanzia enzi za kudai uhuru, wakati wa mfumo wa chama kimoja na kuingia kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa. Kiongozi huyo nikatibu Mkuu wa CUFMaalim Seif Shariff ambaye anatarajia tena kuwa mgombea wa Kiti cha Urais wa Zanzibar kwa mara ya tatu katika Uchaguzi mkuu ujao 2005.

KUJULIKANA KWA MAALIM SEIF
Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi (CUF) ambaye anategemea sana na wafuasi wake kuna haja kumtiza ma kama kweli ana sifa za mwanasiasa na mwanademokrasia wa kweli. Sief Shariff Hamad alianza kujulikana Zanzibar baada ya Mzee Aboud Jumbe Mwinyi kumteuwa kuwa Waziri wa Elimu mwaka 1977 na baada ya kuunganishwa vyama vya ASP na TANU na kuzaliwa CCM.

Maalim Seiff alikuwa mwalimu katika skuli ya Sayyid Abdalla ambayo hivi sasa inajulikana kwa jina la Fedel Castro, ambapo alikwenda kufundisha mara baada yakumaliza masomo yake ya kidatu cha sita katka Skuli King Geoge hivi sasa inajulikana kwa jina la Skuli ya Sekondari ya Lumumba. Alizaliwa Mtabwe katika kitongoji kinachoitwa Nyali, Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba, na kupata elimu yake ya msingi katika Skuli ya Uondwe na hatimaye kumaliza masomo yake ya elimu ya juu katika Skuli ya King Geoge. Mnamo mwisho wa miaka 1960 Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika juhudi ya kuandaa Wataalamu na viongozi wa baadae, iliwapeleka wanafunzi wake nchi za nje kujifunza fani mbali mbali. Seiff, alichaguliwa kuwa miongoni mwa wanafunzi hao waliopelekwa kwa ajili ya kuchukua taaluma katika vyuo vya nchi za nje.
Kwa wakati ule hao wote waliopelekwa nchi za nje walikuwa wanaandaliwa kuwa viongozi na makada watakaoshika nyadhifa mbali mbali za uongozi. Kwa sababu kipindi hicho hakikuwa kirefu tangu kufanyika Mapinduzi yaliyomuondoa Sultan, waliopatiwa nafasi hizo walilazimika waangaliwe kwa kuchunguzwa hasa misimamo yao kisiasa. Seiff katika kuchunguzwa itikadi yake ya kisiasa ikabainika alikuwa na msimamo wa ki-Hizbu tangu alipokuwa Beit-el-Ras. Akiwa bado mwanafunzi alianzisha Chama cha wazawa wa Pemba mapema mwaka1961, Chama hicho kilitumika kukiibia kura Chama cha ZNP (HIZBU) hasa katika Uchaguzi wa mwisho mwaka 1963. Hali hiyo iliwezekana kutokana na MaalimSeiff kuwa karibu sana na Zaim Ali Muhsin, Maulid Mshangama, Ibun Saleh, na Abduirahman Babu. Alishiriki mara nyingi katika mikutano ya siri ya ZNP iliyokuwa ikifanywa na Maulid Mshangama wakati huo alipewa tuzo ya kumuoa mtoto wa kifalme aitwae Amal. Walikuwa kila jioni walienda Beit-EL-Ras kufanya mazoezi ya kutembea ufukweni, huku kila siku Seiff akiwa ndiye aliyekuwa akiwatembeza. Akishirikiana na Ali Muhsi, Seiff aliwahi kuandaa Maulid I Beit-EI-Ras 1963 kwa njama ya kuwakutanisha pamoja Ali Muhsin na Mzee Karume, ambaye walimualika na akahudhuria. Baadaye Seiff alitangaza ASP imeungana na ZNP.Hivyo Chama cha Wazawa wa Pemba kilishiriki kikamilifu katika wizi wa kura wa kiti cha Darajani 1961. Wizi huo wa kura ndio uliokuwa sababu ba chimbuko hasa ia vita vya Juni. Mwak 1963 wakati ASP ilipojidhatiti kukichukua kiti cha Darajani kwa kumueka mgombea wake Mzee Thabit Kombo. Juma Ngwali kwa kushirikiana na chama cha Wazawa wa Pemba, chini ya uongozi wa Seiff walikabidhiwa meli ya Jamuhuri wakati huo ikiitwa Sayid Khalifa (jina la mmoja kati ya Wafalme waliotawala Zanzibar) kwanda kuchukuwa watu Pemba kwa ajili ya kupiga kura kwa Mgombea wa ZNP, na kiti hicho kilichukuliwa na ZNP. Seiff alisikika akijigamba kuwa juhudi zake zimeleta mafanikio. Kutokana na ushahidi huo, jina la Seiff liliondolewa katika orodha ya wanafunzi watakaokwenda kupata mafunzo ya nje yanchi liha ya kuwa alikuwa ameshafika Unguja kwa safari. Ilioekana kuwa sio busara kumrudisha tena Pemba, ndipo ilipoamuliwa apelekwe katika Skuli ya Sekondari ya Lumumba akafundishe. Maalim Seiff Sharifu aliendelea na kazi ya kufuni disha mpaka mwaka 1972 baada ya kifo cha Marehemu Mzee Abeid Amani Karume Rais wa kwanza wa Zanzibar ambapo nafasi yake ikashikiliwa na Bwana Aboud Jumbe. Katika kipindi cha utawala wake Jumbe, wakati huo Waziri wake wa Elimu akiwa Bwana Said Iddi Bavuai na Naibu Waziri Bwana Aboud Talib, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mara ya kwanza ilipeleka wanafunzi kumi na moja kujiunga na Chuo Kikuu cha Dar-es Salaam. Waliteuliwa vijana hao waliofaulu vizuri masomo yao ya kidatu cha sita na kupelekwa Chuoni huko pamoja na vijana hao aliteuliwa na Seiff Sharif yeye akiwa Mwalimu katika Skuli ya Sekondari ya Lumumba. Vijana hao ni -:
1. Abdalla Ismail Kanduru
2. Abubakar Khamis Bakari
3. Aziza Ali Saidi
4. Iddi Pandu Hassan
5. Juma Duni Haji
6. Mabrouk Jabu Makame
7. Mbarouk Omar
8. Moh’d Mwinyi Mzee
9. Omar Ramadhan Mapuri
10. Said Gharibu Bilali
11. Seiff Sharifu Hamadi

Kama kawaida katika kufanya hadhari ya kuteua vijana, Wizara ya Elimu ilikuwa na kazi kubwa ya kufanya uchaguzi juu ya misimamo yao kisiasa, jambo ambalo lilipelekea wajumbe wa Kamati aya Wizara kubishana, hatimae Mzee Jumbe akashauri kuw ani vizuri kusahau tofauti zilizokuwepo za kisiasa na waachiwe vijana wapate elimu ili kuja kulitumikia Taifa.
Wakiwa katika mazingira ya Chuo Kikuu, mawazo ya kutaka kuleta mabadiliko ya maendeleo Zanzibar yaliibuka na kuwatawala vijana hao. Hali ya kutoridhika na baadhi ya mwenendo na maamuzi yaliyokuwa yakichukuliwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibaryaliingia katika vichwa vya baadhi yao. Kutokana na hali hiyo, kulijengwa msimamo na vijana hao kwamba yeyote atakayebahatika kapata nafasi ya juu, ajitahidi kuwavuta wenzake ili wasaidiane katika maendeleo ya haraka.
Baada ya kumaliza masomoa yao, wakiwa wote wamechukuwa shahada ya kwanza ilioambatana na ualimu, isipokuwa watu watatu, Seiff Sharifu alichukuwa Shahada ya kwanza katika Social Science, Iddi Pandu na Abubakar Khamis wao walichukuwa Shahada ya Sheria. Baada ya kumaliza masomo yao walirejea Zanzibar. Naibu Waziri wa Elimu Bwana Aboud Talibu aliongozana nao hadi kwa Rais Jumbe kwa nia ya kumfahamisha kuwa vijana hao wamemeliza masomo yao na wako tayari kulitumikia Taifa. Rais Aboud Jumbe kwa sababu alimkumbusha Seiff Sharifu kwa kuwa aliwahi kumfundisha King Geoge kabla hajaacha kazi ya ualimu na kujiunga na siasa, aliagiza wale wahitimu kumi wapangiwe kazi na Seiff Sharifu akampa kazi Ikulu. Waliobaki mbali ya waliosomea sheria walipewa Chuo cha Ualimu Nkuruma kwa kazi ya kufundisha. Maalim Seiff alifanya kazi kwa uhodari mkubwa mpaka akafikia cheo cha Katibu wa Rais, hadi mpaka pale alipoteuliwa na Rais Jumbe kuwa Waziri wa Elimu wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Kwa maana hiyo aliyemfanya ajulikane Maalim Seiff Zanziba, na hatimae Tanzania nzima, ni Mzee Aboud Jumbe. Na alifanya hivyo kwa lengo la kuimarisha umoja na mshikamano wa Wazanzibar.

AKIWA WAZIRA WA ELIMU
Mtu wa kwanza aliyebahatika kupata wadhifa mkubwa miongoni mwa vijan hao alikuwani Maalim Seiff alipoteuliwa kuwa Waziri wa Elimu. Kwa kiasi Fulani alitekeleza ahadi waliopeana na wenzake kwani aliwavuta Mbarouk Omar na Omar Ramadhan Mapuri wakiwa ni watu wa karibu yake sana na kutokana na kufahamu kuwa anafanya kazi na wenzake Maalim Seiff alianza kujijengea ngome ya kufanya atakavyo kwa kuamini wasaidizi wake hawawezi kumsaliti kutokana na kuwa yeye ndiye aliyewapendekeza kuteuliwa kushika nafasi hizo.

Akiwa Waziri wa Elimu ndipo alipoanza kutekeleza sera za ubaguzi kuwagawa Wapemba na Waunguja . Kila kitu ikiwemo nafasi ya nyingi za mzsomo zilielekezwa Pemba na kuwapa zaidi jamaa zake hasa wa Mtambwe. Alifanya hivyo kwa kuelewa kuwa Serikali imeweka utaratibu mzima wa kuangslia mgao wa nafasi za masomo ya juu kwa sehemu ya Unguja iliokuwa na wakaazi wengi, kupatiwa nafasi sita na Pemba nne kwa kila nafasi 10 zilizopatikana Akiwa Waziri wa Elimu Zanzibar, Maalim Seiff alibadilisha mfumo huo na kuweka nafasi sita kwa Pemba na nne kwa Unguja, tena katika nafasi hizo nne za Unguja, hutafytwa wale wenye asili ya Pemba ambao wanaishi Unguja na kupatiwa nafasi hizo na kukifanya kisiwa cha Unguja kutopata nafasi hata moja.Alipobaini mpango wake huo huenda ungegunduliwa, alibuni mbinu nyengine ya kuwapeleka masomoni katika vyuo vya Bara vijana wa Pemba kwa kuwapeleka vyuoni moja kwa moja bila ya kuwapitisha Wizarani,na Serikali Muungano ilipouliza, Maalim Seiff kwa niaba ya Zanzibar alithibitisha kuwa wanafunzi hao waliteuliwa kihalali na SMZ. Na wengi kati ya wanafunzi waliopelekwa kwa mtindo huo walikuwa hawana sifa za kujiunga na vyuo hivyo. Aidha Maalim Seiff alidiriki kuwaondoa wafanyakazi wenye nyadhifa za juu katika Wizara wenye asili ya Unguja na kuwashusha vyeo na kuwapa jamaa zake wa Pemba. Hali ilipozidi kuwa mbaya na kuchukiza zaidi baada ya Maalim Seiff kuhusika pia na kashfa ya ubadhirifu wa fedha za mradi wa madawati ya Skuli. Ndipo Rais Aboud Jumbe aliparifiwa vlio vya muda mrefu vya wananchi waliokuwa wamechoshwa na vitendo vya upendeleo vilivyokuwa vikifanywa na Maalim Seiff. Rais Jumbe alichukuwa hatua ya kumuondoa katika wadhifa wake huo. Kuanzia siku hiyo Maalim Seiff alianza kujenga chuki dhidi ya Mzee Jumbe, kwa kudai kwamba amemuonea kufuatia kumuondoa katika wadhifa wake waWaziri wa Elimu.

HAMADI NDANI YA CHAMA CHA MAPINDUZI
Kutokana nawadhifa aliokuwa nao wa Waziri wa Elimu Maalim Seiff aliweza kuwa mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, aliitumia vyema nafasi hiyo kwa kuhakikisha kundi lake linaingia katika uongozi wa juu wa Chama Cha Mapinduzi akijua kuwa ndio nguzo pekee atakayoshikilia.Kwa kuwa Maalim Seiff wakati anafukuzwa Uwaziriwa Elimu, alikwishakuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, aliitimia nafasi hiyo kujijenga zaidi na pia kumfitini Mzee Jumbe kwa Mwenyekiti wa CCM Mwalimu Julius K. Nyerere kuwa Mzee Jumbe kwa kushirikiana na waasisi wa ASP na Mapinduzi hawapendi wasomi. Hatimaye Mwalimu Nyerere aliishika fitna hiyo, jambo lilimpelekea Mwalimu kumchukua Maalim Seiff kumuhamisha Bara ambako alimpa kazi ndani ya Chama Cha Mapinduzi. Hapo ndipo Maalim Seiff alipoitumia nafasi hiyo kujijenga kwa Mwenyekiti wa CCM, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na kuwa kipenzi chake.

Akiwa Makao Makuu ya Chama huko Dodoma, ubaguzi aliokuwa nao na kuwapendelea jamaa zake aliendelea nao. Nafasi aliyopewa aliitimia kwa kuwapatia nafasi ndani ya Chama Cha Mapinduzi watu wake kadhaa waliokuwa karibu naye. Kwa sabaubu Maalim Seiff ameshakamata mpini aliitumia nafasi hiyo kumfyeka yeyote ambaye alikuwa hakukubaliana na mawazo yake. Aidha aliendelea tabia ya chuki dhidi ya viongozi waasisi wa ASP, na kumpelekea kuwaona viongozi hao kuwa ni maadui na kuanzisha kuwaandama.

Maalim Seiff aliitumia vyema nafasi hii, na kufanya achaguliwe tena kuwa Mjumbe wa Kmati Kuu ya CCM katika Uchaguzi Mkuu wa Chama Cha Mapinduziuliofanyika mwaka 1982. Mwalimu Nyerere hakumshitukia mapema akampa wadhifa wa kuwa Katibu wa Halmashuri Kuu ya Taifa akiongoza Idara ya Uchumi katika Sekretarieti hiyo ya NEC. Akiwandani ya Sekretariet, Maalim Seiff alifanya kazi ya kuichimbai Serikali ya Zanzibar kwa kuendelea kumuandama Mzee Aboud Jumbe kwa kushirikiana na watu wake aliofanikiwa kuwapenyeza ndani ya Chama Cha Mapinduzi.

Wakati huo walikuwa wameshaunda kikundi cha siri walichokuwa wanakiita PEMBA LEBERATION ORGANAIZESHENI (PLO)uhudi ya Maalim Seif na wenzake zilifanikiwa kumuangusha Mzee Jumbe baada ya kujenga hoja kuwa Mzee Jumbe anataka kuvunja Muungano wa Tanzania. Walifanikiwa kwa siri kupata waraka wa mapendekezo ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar yaliyokuwa ywasilishwe mbele ya Halmashauri Kuu ya Taifa kuhusu muundo wa Muungano wa Serikali tatu. Maalim Seif na wenzake walidai kuwa Mzee Jumbe anataka Muungano wa Serkali tatu (3). Hii nathibitika pale waraka huo ulipowasilishwa na mmoja ya Mawaziri wa SMZ mbele ya Kamati Kuu Baadhi ya vijana wa Zanzibar wakiongozwa na Malim Maalim Seif walioshikilia kuondoshwa kukodishwa madarakani Mzee Jumbe. Wakati mmoja wa Mawaziri wake wa karibu alipokataa shauri hilo, walimuandama kwa kumwambia kuwa yeye ni kibaraka wa MMzee Jumbe na alifika hatua ya kutishiwa hata maisha yake kwa kuambiwa kuwa atauliwa. Mjumbe mmoja wa Kamati Kuu mwenye asili ya Pemba aliasa kwa kuwambia wajumbe wenziwe wasiwe na haraka, kwani Mzee Jumbe kama binaadamu siku moja ataacha madaraka kwa njia moja au nyengine. Mbele ya Halmashauri Kuu ya CCM, Maalim Seif na wenzake walimuadhiri Mzee Jumbe. Pamoja na madai ya kutaka kuvunja Muungano pia walifanikiwa kuwadanganya wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa kutoka Bara, kuwa Mzee Jumbe alikuwa anataka kutumia “Revolution Justice” yaani hukumu za Kimapinduzi dhidi ya watu walioitwa wakorofi wa Zanzibar. Ukweli ni kuwa Mzee Jumbe alikwisha pata habari za kuundwa kwa (PLO) iliokuwaya wahusia wa kundi hilo walidhibitiwa ambao wengi wao walikuwa wakijiita kuwa ni waislamu wenye msimamo mkali.

Kutokana na kadhia hiyo, Mzee Jumbe alilazimika kujiuzulu nafasi zake zote za uongozi wan chi. Ndipo alipoteuliwa bwana AliHassanMwinyi kuwa Rais w muda wa Zanzibar mwaka 1984.. Baada ya kuteuliwa Mzee Ali Hassan Mwinyi kushikilia nafasi hiyo, Mwalimu Nyerere kwa kumuamini Maalim Seif, alimuomba Mzee Ali Hassan Mwinyi amchuue Maalim Seif ili awe Waziri Kiongozi wake apate kumsaidia kutuliza hali ya hewa iliyochafuka Zanzibar. Maalim Seif alirejea Zanzibar bila ya kuzingatia kilichopelekea kufukuzwa kwake katika wadhifa wa Waziri wa Elimu.

Baada ya kuapishwa tu Maalim Seif Sharifukuwa Waziri Kiongozi, alijionesha wazi hali halisi aliyinayo.Kwani hapo ndipo alipodhihirisha kuwa yeye ni chuikatika ngozi ya kondoo, kwani alilihutubia Baraza la Wawakilishi, kwa kutoa Hutuba ambayo asili mia moja (100%) ilikuwa inadhihirisha unafiki wa kiongozi huyo kwa kulinganisha na vitendo vyake vya sasa. Sehemu ya kwanza ya Hutuba hiyo, ilichapishwa katika Gazeti la Ijumaa Machi 9, 1984. na sehemu ya pili ilifuata toleo la siku ya pili yake.
Jambo jengine alilolifanya Maalim Seif wakati akiwa Waziri Kiongozi ilikuwa ni kuwaachilia waliodhibitiwa kwa kuhusika kwao na madai ya uhaini. Vijana hao walioachiliwa hivi sasa ni watu wake wa karibu katika shughuli za kisiasa.

Mzee Mwinyi katika kipindi chake kifupi akiwa na Maalim Seif alimstahamilia mambo mengi kwa sababu alijifanya kama yeye ndiye Rais wa Zanzibar ikiwa ni pamoja na kupendekeza kuwekwa Wakuu wa Mikoa wa Wilaya pamoja na vikosi vya Ulinzi vya (SMZ) watu kutoka Pemba ambako katika uendelezaji wwa mipango yake ya ubaguzi kati ya wazaliwa wa Unguja na Pemba. Kwa tabia yake hiyo ndio maaana maamuzi yote yalikuwa yakitolewa na Serikali alijifanya yanatokana na yeye.

Mara kadhaa amekuwa akijigamba kuwa yeye ndiye aliyeanzisha utaratibu wa ulegezaji wa masharti ya biashara Zanzibar. Ilionekaana hivyo ingawa ukweli ni kuwa mara baada ya kushuka kwa kiasi kikubwa Uchumi wa Zanzibarkutokana na kuanguka kwa bei ya zao la karafuu mwanzoni mwa miaka ya 1980, Mzee Jumbe ndiye aliyepeleka kwenye Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi mpango wa ulegezaji masharti ya biashara ili kuinusura Zanzibar na hali ngumu ya Uchumi. Hadi Mzee Jumbe anajiuzulu, mpango huo ulikuwa umeshapitishwa na NEC bado utekelezaji wake ambapo Mzee Mwinyi alipoingia madarakani aliukuta uko juu ya meza na kuanza kuutekeleza.

Hata hivyo Maalim Seif alijitangazia mpango huo ameubuni yeye. Aidha alijitangazia kuwa msaada wa ujenzi wa uwanja wa michezo wa Gombani umetokana nay eye ingawa aliyekwenda Jamhuri ya Watu wa Korea kuomba msaada huo alikuwa ni Mzee Mwinyi.

Tabia hiyo ya kujitapa imechangia kuengea kasi ya kunawiri kwa mtengano wa Ki-kabila na Umajombo wa Upemba na Unguja, na ukazidi kupamba moto kwani Wapemba waliamini kuwa haya yote yameletwa na jamaa yao.

Akiwa Waziri Kiongozi alikuwa akipita katika ofisis za Serikali na pindi akibaini kiongozi katika sehemu hiyo bado hajafika zaidi akihakikisha kwamba nafasi hiyo inashikiliwa na mtu wa Unguja, alikuwa akimtimua na badala yake kumweka jamaa yake. Unyanyasaji kwa watu wa upande mmoja wa Zanzibar ulizidi sana. Mfano ulio hai inadhihirisha kuimarika kwa ubaguzi ndani ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ni kwamba Maalim Seif alikuwa hana nafasi ya kukutana na mtu wa Unguja wakati jamaa zake walikuwa hawatoki ofisini na nyumbani kwake.

Chini ya usimsmizi wake alshiriki kuwanyang’anya magari yao na vitu vyengine wafanyakazi wa Meli ya M.V. Mapinduzi waliyoyanunua baada ya kujinyima wakati walipokuwa Japan ambako meli hiyo ilikwenda kufanyiwa matengenezo. Aliweza kulitekeleza hilo akijua kuwa kati ya wamiliki wa magari hayo hakuna jamaa yake.
Kwa kuwa Mzee Ali Hassan Mwinyi wakati huo akiwa Rais wa Zanzibar, alikuwa akisisitiza kuwa “Zanzibar ni njema atakae aje” Maalim Seif aliitumia nafasi ile kuwarejesha wale wote waliotamani kurudi Zanzibar ambao walikimbia baada ya Mapinduzi ya 1964.
Wengine alidiriki hata kuwarudishia baadhi ya mali zao zilizotaifishwa kisheria baada ya Mapinduzi ya Januari, 12.1964 ikiwa ni pamoja na kuwarejeshea nyumba zao watu waliorudi Zanzibar. Alitamani kuwarejashea wenyewe hata yale mashamba yalichukuliwa na Serikali, na kuwagaiya wananchi Eka tatu tatu. Katika kuendeleza mpango wake, Maalim Seif aliiandaa Waraka ambao aliuwasilisha kwenye Kikao cha Halmashauri Kuu ya taifa ya Chama Cha Mapinduzi unaoeleza dhamira ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuwanyang’anya wale wote waliopewa mashamba hayo baada ya Mapinduzi na ambao wanashindwa kuyaendeleza, na kugawiwa kwa wale wenye uwezo wa kuyaendeleza.Hapa Maalim Seif aliweka mtego na kama angelifanikiwa nia yake ilikuwa ni kuwanyang’anya wananchi eka tatu zao za ardhi walizopewa na Serikali ili ardhi hiyo wrejeshewe Mabepari waliokuwa wakihodhi kabla ya Mapinduzi ya januari, 12.1924. Alifanya hivyo akijua kuwa kunatofauti ya uwelewa kati ya wananchi wa Tanzania Bara na wa Zanzibar juu ya dhana ya mashamba. Kwani kwa Tanzania Bara, mashamba huwa hata yale ya anayolimwa mahindi na viazi ambayo hayana mazao ya kudumu. Hivyo baadhi ya viongozi wa Chama Cha Mapinduzi ambao walikuwa wajumbe wa kikao hicho wakamueleza Mwalimu Nyerere kuwa mashamba yaliyokusudiwa katikawaraka husika ni eka tatu walizopewa wananchi na Serikali baada ya Mapinduzi, wala si mashamba ya mahindi, maharage na viazi. Mashamba hayo yana miti ya kudumu na kati ya miti ya hiyo mengine imepandwa na wenyewe wananchi waliopewa ardhi hiyo. Aidha wengine kati ya wananchi hao wamejenga nyumba zao na wanaishi humo na familia zao. Kwa hoja hizo waraka huo ulikataliwa. Lengo la Maalim Seif lilikuwa ni kuwanyanga,nya ardhi wananchi wanyonge wa Zanzibar.

Maalim Seif alikwepa kuupeleka waraka huo kwenye kikao cha Baraza la Wawakilishi akijua fika ndani ya kikao hicho baadhi ya wajumbe wangegundua mpango wake na wasingekubali. Matokeo Mwalimu Nyerere akatoa uamuzi kuwa ardhi iliyogawiwa wananchi mara baada ya Mapinduzi ya Januari 12, 1964 iachwe kama ilivyo.

HAMADI KUSHINDWA URAIS WA ZANZIBAR KWA MARAYA KWANZA 1985
Kama ilivyo katika Katiba ya Zanzibar wakati Rais wa Zanzibar akiondoka madarakani kwa njia yoyote ile, atateuliwa zanzibari mwengine kushikilia wadhifa ho kwa muda wa siku tisiini, na wakati huo Uchaguzi wa Rais utaitishwa ili apatikane Rais aliyechaguliwa na wananchi ili amalizie kipindi kilichobaki. Wakati Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM, ilipokaa kupendekeza jina la Mgombea Urais wa Zanzibar,kwa mujibu wa Katiba ya CCM, Kamati Kuu inateua majina ya wazanzibari wawili kupeleka kwenye Halmashauri Kuu ya Taifa, na kupigiwa kura. Mshindi katika watu hao wawili ndie atakaekuwa mgombea aliyeteuliwa na Chama kwenda kupigiwa kura na wananchi. Kwa kuwa wakati ule Mzee Mwinyi ndiye aliyekuwa anashikilia kiti cha Urais wa Zanzibar, hivyo jina lake lilikuwa la kwanza kuzingatiwa. Kamati Kuu imependekeza mzanzibari mwengine ili kukamilisha majina mawili nae ni Mzee Idrisa Abdulwakil, wakati huo akiwa Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar. Mzee Idrisa alifanya kitendo cha kiungwana kilichowapelekea watanzania wotngaa, kwani Mzee Idrisa aliondosha jina lake katika kuwania nafasi ile na kumwache kushangaa, kwani Mzee Idrisa aliondosha jina lake katika kuwania ile na kumwachia MzeeMwinyi kupita bila ya kupingwa. Chama kikamteua Mzee Mwinyi kuwa Mgombea nafasi ys Urais wa Zanzibar, Uchaguzi ukafanyika na Mgombea huyo alichaguliwa kwa kura nyingi Unguja na Pemba.

Katika uchaguzi mkuu wa mwka 1985 baada ya Mzee Mwinyi kupendekezwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, nafasi ya mgombea Urais wa Zanzibar ilikuwa wazi. Hivyo ikabidi Chama kitafute mgombea mwengine. Kamati Kuu katika kipindi hiki ilimpendekeza tena Mzee Idrisa. Kwa hivyo jina la Mzee Idrisa likawa la kwanza, na kazi ikawa kutafuta jina la Mzanzibari wa pili. Kama kawaida yake Hamadi jinsi anavyopenda madaraka, na kwa kuwa nafasi hiyo alikuwa akiinyemelea kwa muda mrefu, kwa vile alikuwemo ndani ya Kamati Kuu. Aliitumia nafasi pale Mwalimu Nyerere ambae alikuwa ndie Mweyekiti wa Kikao alipotania kwa kusema “ Nani atamshindikiza Mzee? Hapo aliinuka Maalim Seif bila ya aibu na kusema “Mie´ Na kikao kikaunga mkono kwa kupiga makofi huku wajumbe wakidhani kuwa Hamadi ni muungwana kama alivyo mzee Idrisa. Kujipendekeza kwake kungekuwa na lengo la kuondosha jina kama alivyofanya Mzee Idrisa wakati alipokuwa yeye na Mzee Ali Hassan Mwinyi, ili kukiepusha Chama kuwa mgawanyiko kutokana na jambo hili. Hapo Kamati Kuu ikatoka na majina mawili la Mzee Idrisa Abdulwakil na Maalim Seif Sharrif Hamad, ambayo yalipelekwa kwenye kikao Halmashauri Kuu, kwa kupigiwa kura na mshindi atakuwa ndie mteule wa Chama Cha Mapinduzi kugombea nafasi ya Rais wa Zanzibar. Inasemekana kuna kijana mmoja miongoni mwa wajumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa alimtania Seif, na kumuuliza. “Eti nasikia umeamua kumshindikiza Mzee?” Maalim Seif alijibu. “Kumshindikiza maana yake nini? Mimi nagombea”. Kauli hii ya Seif ikawafanya baadhi ya vijan wenye uchungu na nchi kufanya kazi ya ziada kumfanyia Kampeni Mzee Idrisa. Na Seif nae na kundi lake kwa uapande wake wakakazana kufanya Kampeni ili kuhakikisha mtu wao anashinda nafasi hio. Kampeni zilikuwa ngumu sana, kwani kundi la Seif Shariff lilijidhatiti kufanya Kampeni za kumpaka matope Mzee Idrisa hasa mbele ya wajumbe wa Halmashauri Kuu kutoka Mikoa ya Tanzania Bara. Miongoni mwa Kampeni yao kubwa ni kuwa huyu ndie miongoni mwa wazee wa Zanzibar wasiopenda mabadilikko na wasiowapenda wasomi. Na kwa upande wa vijana wanamapinduzi wa Zanzibar wakakaza kamba ya kuhakikisha Mzee wao anafanikiwa kwani wakijua kuwa nafasi hio pindipoikiingia kwenye mikono ya mpinga Mapinduzi, Mapinduzi yao yatakuwa hatarini. Wakati wajumbe wakiwa ndani ya ukumbi wa mkutano, karatasi za kupigia kura zimeshaandaliwa, katika kutawanya kuratasi hizo zenye maelezo binafsi ya wagombea, ambazo ziligunduliwa na kasoro katika kuziandaa. Kasoro hizo ni kuwa mgombea Seif Shariff kuwa na maelezo marefu yanayoelezea sifa zake, wakati Mzee Idrisa alipewa nafasi ndogo ya maelezo binafsi. Sifa na nyadhifa nyingi alizowahi kushika ndani ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar mara baada ya Mapinduzi, na Serikali ya Jamhri ya Muungano baada ya kuzaliwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, hazikuelezwa. Hata lile tukio kubwa alilolifanya la kuacha kazi ya ualimu kwa hiyari yake, na kujiunga katika kundi la wapigania Uhuru kwa upande wa ASP nalo pia halikuelezwa. Vijana ndipo walipomwendea Mzee wao bwana Thabit Kombo kumueleza juu ya njama ile ilioandaliwa na Seif Shariff kupitia watu wake aliowapandikiza kwenye Chama kwa. Hivyo baada tu, ya kuanza kikao kijana mmoja alijichomoza kutoa taarifa mbele ya kikao juu ya kasoro hiyo. Na baadaa ya taarifa hiyo Mzee Thabit Kombo alinon’gona na Mwenyekiti wa kikao. Mwenyekiti alilazimika kukiakhirisha kikao kwa muda ili kusawazisha kasoro zilizojitokeza. Mwenyekiti aaliagiza kasoro zilojitokeza zisawazishwe na wagombea wote wawepo kwenye kikao, na kila mmoja apewe nafasi ya kujieleza mwenyewe.

Baada ya kupigwa kura na kuhesabiwa, Mzee Idrisa alimshinda Maalim Seif kwa kura 7, na alitangazwa na CCM kuwa Mgombea Urais wa Zanzibar katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 1985. Kwa kuwa Maalim Seif alishindwa kuheshimu matokeo yale na kuanza kudai kuwa, amenyang’anywa nafasi yake ya kugombea urais wa Zanzibar, na hakupewa nafasi hiyo kwa sababu yeye ni Mpemba. Alieleza bayana kwamba alishinda lakini ameibiwa kura, na alisingizia kuwa Demokrasia na haki haikutendeka katika uchaguzi na kusingizia mambo kadhaa.

Kitendo hicho kilimjengea sifa mbaya na kuonekana kuwa ni kiongozi mwenye tabia mbaya ya ubinafsi na chuki na hasa alipoanza kujenga chuki kwa vijana wote aliowadhani kuwa hawakumuunga mkono.

Mwalimu Nyerere alibaini kuumia kwa Maalim Seif kutokana na kuikosa nafasi hiyo, hivyo alijaribu bila mafanikio kumpoza mpoyo kwa kumtaka awe na subira, na kumsisitiza aende Zanzibar kumpigia kampeni Mzee Idris, ili kuhakikisha anachaguliwa kwa kura nyingi.

Hata hivyo, Maalim Seif hakuzingatia ushauri na maelekezo aliyopewa na MwalimuNyerere. Alichokifanya Maalim Seif badala yakr ni kukusanya nguvu za kundi lake lililokuwa likimuunga mkono, muja Zanzibar kupiga kampeni dhidi ya maamuzi ya Chama. Alijidhatiti kuhakikisha Mzee Idris hachaguliwi kuwa Rais wa Zanzibar.

Wakati w harakati za kampeni Maalim Seif na wenzake, wengi wao wakiwa ni wazaliwa kutoka Pemba, walielekeza nguvu zao Pemba na kuhakikisha Mzee Idrisa hachaguliwi. Wananchi na hasa wa Pemba, walitiwa maneno ya fitna na kutakiwa wasimpigie kura Mzee Idris kwa kudai kuwa nafasi ya Urais wa Zanzibar safari hyo ni zamu ya watu wa Pemba, ila watu wa Unguja wanang’ng’ania tu kwa sababu wanawachukia wapemba. Iliendelezwa kampeni kwamba katika uchaguzi wa kutafuta Mgombea uliofanywa ndani ya Halmashauri Kuu ya Taifa, Maalim Seif ndiye aliyeshinda, lakini amedhulumiwa kwa kuibiwa kura.

Aliwaambia watu wa Pemba wasimchague Mzee Idris kwa sababu anawachukia wapemba, pindipo wakimchagua kuwa Rais wa Zanzibar atawaadhibu wapemba. Wpiga kura walishawishiwa kwa kuambiwa kuwa, kwenye karatasi ya kupigia kura pale palipo kuwa na ukuta nyuma yake kuna picha ya MaalimSeif, hivyo watakaopiga kura zao kwenye Ukuta watakuwa wamemchagua Maalim Seif. Maalim Seif alifanya hivyo kwa kuamini kuwa pidipo wananchi watakapo piga kura zao kwenye ukuta, na ikiwa Mzee Idriss atashindwa kupata kura za kumuwezesha kuchaguliwa, kwa mujibu wa katiba ya Chama italazimika vikao vya chama kukaa tena na kufikiria jina la mwanachama mwengine ili agombee nafasi hiyo. Na kwa fikra zake aliamini kuwa lingefikiriwa tena jina lake.

Maalim Seif na kundi lake waligawana kazi hiyo wengine Unguja kwa mbinu zao na wale wa Pemba wakiongozwa nay eye mwenyewe. Na kwasababu Maalim Seif ni mpemba na alikwisha wajaza kasumba wapemba wenziwe, kuwa wasimchgue Mzee Idris, matokeo ya Uchaguzi ule yalikuwa mabaya sana kwa Pemba, tofauti na hali ilivyokuwa Unguja. Matokeo mabaya ya Pemba hayakuathiri ushindi wa Mzee Idris kuchaguliwa kuwa Rais wa Zanzibar mwaka 1985. Hapa nataka kueleza kitu kimoja. Seif alipoelekea Pemba na kutia fitina kuwa ameonewa na kura zake zimeibiwa. “Siku zote mwizi hudhani watu wote ni wezi kama yeye. Na dhalimu siku zote hudhani kuwa watu wote ni Madhalimu kama yeye.” Lakini pamoja na njama zote hizo, hatimae Mzee Idriss alitangazwa kuwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Pamoja na matukio yote hayo, Mzee Idris baada ya kuchaguliwa alimteuwa tena Maalim Seif kuwa Waziri Kiongozi. Rais Idriss alimpa Seif haki zake zote, ikiwa ni pamoja na kumshauri katika kuunda Baraza la Mawazir. Maalim Seif aliitumia nafasi hiyo kama kawaida yake kupandikiza watu ambao wangetenda vyo vyote vile atakavyo yeye.

Kwa kuwa mambo aliyoyafanya Maalim Seif kwa kushirikiana na kundi lake haya kuwa siri, na yalikuwa kinyume na maadili ya CCM viongozi wa CCM wa Zanzibar walilijadili jambo hilo kataka vikao mbalimbali hadi kufikia katika kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa kilichofanyika mara baada ya Uchaguzi huo, kwa kufany tathmini ya matokeo ya uchaguzi. Katika kulijadidi jambo hilo moja kwa moja Maalim Seif na kundi lake walionekana kuwa na makosa.

Lakini aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mwalimu J.K. Nyerere akitumainia kuwa Seif Shariff aliyafanya yale kutokana na joto la Uchaguzi tu, alikiomba kikao kimsamehe huku akidhani kuwa Seif Shariff atajirekebisha na kumapa ushirikiano wa kutosha Mzee Idris hasa kwa kuzingatia kuwa amekosa Urais lakini amepata Uwaziri Kiongozi.

Pamoja na kuwa Mwalimu Nyere, alishauri jambo hilo liachiliwe mbali, lakini mambo hayakuwa kama yalivyotarajiwa. Matokeo yake Seif Shariff na kundi lake walikuwa kama samba aliyewahi kula nyama ya mtu. Hawasikii wala hawaoni, akili zao zote zililenga kwenye nafasi ya Urais tu. Walianza kufanya vituko vya nuni Firauni. Kwanza walifanya kila mbinu ili kuhakikisha Mzee Idris inashindwa kuitawala Zanzibar. Walijipanga katika kila nafasi nyeti za kuongoza nchi. Kuanzia Uwaziri, Ukuu wa Mkoa Ukatibu Mkuu, Ukurugenzi, Umeneja hadi uafisa wa Serikali katika Wizara na Taasisi zake.

Walimsokota Mzee Idris asipate pumzi. Baraza la Mawaziri lilikuwa limegawika sehemu mbili, moja iliyomuunga mkono Rais na ya pili iliyomuunga mkono Waziri Kiongozi. Barazala Wawakilishi nalo halikadhalika. Kulikuwa na Wawakilishi wa Rais na wa Waziri Kiongozi. Hata chama cha Mapinduzi upande wa Zanzibar nacho kiligawika sehemu mbili, kulikuwa na viongozi na watendaji waliomuunga mkono Mzee Idris na vile vile walikuwapo wengine waliomuunga mkono Seif Sharuff. Kwa jumla hali ya hewa ya kisiasa Zanzibar ilichafuka.

Seif Shariff alihakikiha kwamba anamjengea uadui Mzee Idrisa hata kwa wale wananchi anaowateua kuwapa dhamana mbali mbali ndani ya Serikali yake. Maalim Seif aliijenga tabia ya kujionesha mwema kwa kila mtu mbaye Rais alikuwa anataka kumkabidhi dhamana ya uongozi au utendaji katika Seriksli.

Silaha kubwa aliyokuwa akiitumainia, ni kuwaelezea watu hao yeye amewapendekeza kushika nafasi za uongozi na utendaji fulani, lakini Mzee Idris hataki. Alikuwa akiwauliza. “Jee, mmekosa nini Mzee? Bila shaka jawabu itakayopatikana hapo ni kushangaa. Kwa sababu pengine baadhi ya wananchi hao hata hawajawahi kukutana na Rais mwenyewe. Hapo Seif huendeleza fitna zake kwa kuwambia watulie kuwa atahakikisha wanateuliwa hata kama Rais hapendi.

Tabia hii iliwafanya wafuasi wa Seif kuamini kuwa yeye ndiye Rais, walifikia hatua ya kubadiliisha jina la tatu la Rais ‘NOMBE” na kuliita “NG’OMBE” huku wakishadidia kwa kusema “Ngo’ombe sasa anamfuata mchungawe.” Yaani Mzee Idrisa anamfuata Seif Shariff kwa kila alitakalo. Kadhia hii ilimpelekea washauri wa serikali kumshauri kuacha kutumia jina hilo la tatu kwa maudhi na karaha aliyokuwa akifanyiwa.

Lengo la Seif Shariff na kundi lake lilikuwa ni kuhakikisha kila aliyekabidhiwa madaraka ndani ya Serikali anaunga mkono kundi lao.

Maalim Seif na kundi lake walichukua ahadi kwamba watawaangamiza waasisi wote wa ASP. Katika kutekeleza azma hiyo, lilianza kwa kuandaa njama za kumuhusisha aliyekuwa Waziri wa kilimo bwana Hassan Nassor Moyo na Naibu wake bwana Abdulla Rashid na tuhuma za ubadhirifu wa fedha za mradi wa Makurunge. Hoja hiyo iliwasilishwa kwenye kikao cha Baraza la Wawakilishi na kundi hilo. Ukumbi ulikuwa moto, kwani baadhi ya wajumbe walisimama kidete kuwatetea bwana Hassan Nassor Moyo na bwana Abdulla Rashid. Kwa sababu walikuwa wanatetea msimamo wa kisiasa dhidi ya siasa za upinzani zilizojengeka ndani ya fumo wa Chama kimoja cha siasa, siri zilizokuwa hazifahamiki na wengi za Seif Shariff na jamaa ziiibuka. Hivyo Seif Shariff aliona mambo huenda yakaharibika, kwa kutumia wadhifa alikuwa nao wa Waziri Kiongozi haraka akaituliza hali hiyo ili kuepuka kuyaweka mambo yao hadharani.



Katika mtizamo wa suala la kuendeleza sera za Chama, Hamad licha ya kukabidhiwa Idara ya Uchumi ya Sekretarieti ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM lakini alikuwa akiendesha mambo yake kinyume na maelekezo ya sera hizo. Kutokana na tabia hiyo ya kuwa ndumila kuwili akiwa na nafasi ya Uwaziri Kiongoziii alikwaruzana na Marehemu Jamal Ramadhani Nassibu kuhusu waraka ulikuwa na kurasa 25 unaoelezea historia ya ukombozi wa Mzanzibar.

Waraka huo uloandikwa na mzee Jamal Ramadhani Nasibu, na kuwasilishwa katika Semina ya Halmashauri Kuu za CCM Mkoa wa Mjini na Magharibi na Wilaya zake wakati huo Mzee Jamal akiwa ni Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM Mkoa wa Mjini Magharib Unguja.

Kilichoonekana wazi ni kwamba katika kutekeleza majukumu yake kama Waziri Kiongozi Seif Shariff hakujali kazi alizokabidhiwa na nchi, bali aliitumia nafasi hiyo kujitafutia nafasi kubwa zaidi. Hakupenda kukaliwa na mtu juu yake. Ndio maana akatumia juhudi na uhodari wake wote kujitafutia Urais kwa njia yoyote ile. Seif na kundi lake waliendesha ufisadi katika nchi.

Seif alifanya kila aliloweza kuhakikisha Zanzibar haiendi mbele. Mali za serikali anazigawa kwa jamaa zake bila ya kujali kuwa ile ilikuwa ni mali ya wananchi. Aliandaa utaratibu uliyohakikisha nyumba za Serikali wanauziwa jamaa zake kwa bei sawa sawa na bure. Mali za Serikali ziliuzwa kwa bei ndogo zisizolingana na thamani ya mali zenyewe. Alitoa viwanja kiholela tu, mashamba ya Serikali yalitolewa kwa jamaa zake na pesa za Serikali zilikopeshwa kwa jamaazake bila hata kufuata taratibu na sheria za mikopo. Mashirika na miradi mbalimbali ya Serikali yalikabidhiwa watu ambao waliyahujumu bila ya hata kujali. Mfano hai ni kukabidhiwa kukiongoza kiwanda cha Maziwa kiliopo Maruhubi mtoto wa dada yake nae alifanya ubadhirifu wa hali ya juu jambo lililopelekea shamba la Ngo,mbe pamoja nakiwanda hicho kuangamia.

Baad ya baadhi ya viongozi walipoona nchi inaelekezwa siko ndipo walipochukua hatua ya kutoa taarifa kwenye vikao vya Chama kuanzia ngazi za chini na hatimaye kufikia kwenye Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi. Na matokeo yake mnamo mwaka 1987 wakati Halmashauri Kuu ya Taifa ya C.C.M. (NEC) ilipokaa katika kikaoo cha kujadili majina ya wana CCM walioomba uongozi katika ngazi za Wilaya, Mikoa hadi Taifa. Taarifa hizo ziliweza kusaidia na kupekea baadhi ya waomba uongozi wa ngazi hizo kutoka Zanzibar kutokuteuliwa kugombea nafasi hizo. Miongoni mwa hao ni:-

Ali Haji Pandu
Shaaban Khamisi Mloo
Khatibu Hassan na
Suleiman Seif Hamadi

Seif Shariff alisalimika kwa sababu ya heshima ya ujumbe wa Kamati Kuu, na nafasi aliyokuwa nayo ya Uwaziri Kiongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Lakini nae hatima yake ilimalizika kwa kukosa nafasi ya kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM.

Maalim Seif alidhamiria hasa kuendeleza upinzani akiwa ndani ya Serikali na ndani ya Chama Cha Mapinduzi. Baada ya kufanikiwak kuwateka viongozi na watendaji wa Chama na Serikali na kutokana na uchungu wa kuikosa nafasi ya ujumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, ndipoalipoamua kupinda mgongo kwa juhudi na maarifa kuhakikisha azma yake ya kuparaganya nchi inafanikiwa. Ndipo baada ya kumaliza harakati za Uchaguzi Mkuu wa Chama wa mwaka 1987 Maalim Seif aliomba ruhusa ya kwenda Matibabuni Ulaya na Rais Idrisa akamruhusu, kumbe huku nyuma tayari chungu kinachochewa moto unarindima nacho kinatokota. Aliwaandaa baadhi ya viongozi wa Serikali wakiwemo Mawaziri, Wkuu wa Mikoa na Wilaya, Makatibu wa CCM wa Mikoa na Wilaya, na kuwataka wamuandalie mapokezi makubwa nay a aina yake.

Mapokezi ambayo hajapata kupokelewa kiongozi yeyote hapa Zanzibar. Waliyaandaa mapokezi hayo kwa makusudi wakaamua kuwa yafanyike Pemba. Maalim Seif alirejea na alikaa Unguja kwa siku mbili tatu na mambo yalipokuwa tayari alikwenda Pemba, huku akimuaga Rais Idrisa kuwa anakwenda kupumzika. Alipofika Uwanja wa Ndege wa Karume Chake Chake Pemba Maalim Seif alilikuta alilolitarajia kwani kulikuwa na ummati mkubwa mno ambao ulikuwa unamngojea na kumpokea. Wengi wa watu hao hawakuwa wakijua nini kinachoendelea, kwani wao waliona kuwa Waziri Kiongozi wao amerejea kutoka matibabuni wanampokea. Baada ya kuteremka kwenye ndege na kusalimiana na viongozi na kutoka nje ya uwanja, palikuwa na Sheikh tayari ameandaliwa na hapo hapo ikasaliwa sala Maalum ya RAKAA mbili ili kumuombea dua Maalim Seif na kumuondoshea “DAFA-EL-BALAA”.
Kwa wale waliokuwepo siku hiyo wanasema Sheikh aliyeteuliwa kuomba dua baada ya sala ya rakaa mbili, aliomba dua kwa kusema: “Kama kiongozi huyu ana kheri na sisi basi Mwenyezimungu tuekee , la kama kiongozi huyu hana kherti na sisi basi utuondoshee”. Baada ya kumaliza dua hiyo, msafara wa miguu ulianza kuelekea mjini Chake Chake kwa maandamano, Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya, Wenyeviti wa Chama wa Mikoa na Wilaya pamoja na mwenyewe Maalim Seif wakiongoza maandamano hayo. Nyimbo zilizokuwa zikiimbwa katika maandamano hayo zilikuwa ni za matusi na kashfahasa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Zanzibar pamoja na watu wenye asili ya Bara. Maneno ya nyimbo hizo yalikuwa Hatuyataki machogo; hatumtaki ng’ombe; hatuutaki Muungano; n.k.

Pamoja na hayo, Maalim Seif alidiriki kumfanyi kitendo kikubwa Mzee Idris kilichodhihirisha dharau, utovu wa nidhamu na udhalilishaji. Kwani wakati wa kipindi chake cha Urais Mzee Idris alipanga kwenda kufanya Ziara Pemba, aliondoka Unguja yeye na msafara wake kwa kutumia usafiri wa ndege hadi Pemba. Alipofika Pemba aliikuta Ikulu imefungwa kwa kufuli, na wakati huo Ikulu ilikuwa ikiiangaliwa na kutunzwa na Mkuu wa Mkoa. Aliyekuwa akishikilia nafasi ya Mkuu wa Mkoa wa Kusini Pemba wakati huo alikuwa ni Maalim Juma Ngwali Kombo, mtu aliyepandikizwa na Maalim Seif kwa madhumuni niliyokwisha kuyataja huko nyuma.

Maalim Seif alimuamrisha Mkuu wa Mkoa afunge Ikulu na aondoke pamoja na funguo zote, kwani hakupenda Rais Idris aende kufanya kazi za nchi katika kisiwa cha Pemba. Jambo ambalo lilimpelekea Mzee Idris kupata usumbufu mkubwa na hatimaye aliamua kurudi Unguja bila ya kufanya kazi alizozikusudi. Jambo hili lilimsikitisha sana Mzee Idris, na kusikika akisma hadharani. “Huyu Seif anataka nini? Kama ni urais si asubiri, mimi bado miaka miwili tu, nimalize muda wangu. Nikimaliza kipindi hiki tu ninamuachia yeye. Hiyo ilikuwa mwaka 1998.

Kutokana na matukio niliyoyataja na mengi menginyo yaliyofanywa na Seif Shariff na kundi lake huko nyuma, Chama cha Mapinduzi kwa makusudi kiliamua kuwaleta baadhi ya Watendaji wa Wilaya na Mikoa kutoka Tanzania Bara kuja kufanya kazi za Chama katika Mikoa na Wilaya za Zanzibar.

Watendaji hao waliotoka Bara kuja kufanya kazi za Chama Zanzibar walishuhudia kwa macho yao matendo ya kuvuruga Umoja na Mshikamano wa Chama cha Mapinduzi hapa Zanzibar vilivyokuwa vinafanywa na Maalim Seif akishirikiana na wafuasi wake.

Mzee Idriss, baada ya kuchoshwa na vitendo vya Seif Shariff na wafuasi wake ndipo alipoamua kulivunja Baraza la Mawaziri na kuliunda upya. Katika hatua hiyo aliyoichukua Seif Shariff alimfukuza Uwaziri Kiongozi, lakini wale Mawaziri wengine wote aliwarudisha kwenye nafasi zao za Uwaziri. Rais Idris alimteua Dr. Omar Ali Juma kuwa Waziri Kiongozi wa SMZ badala ya Seif Shariff Hamad. Hapo Mzee Idris alikuwa kama aliyeongeza Petrol katika moto unaowaka. Wafuasi na wapenzi wa Seif Shariff wakadai kuwa Mzee Idris amemuonea Maalim Seif, amemnyang’anya Uwaziri Kiongozi wake. Alimuradi Nchi iliingiwa na mtafaruku. Lakini kutokana na hekima na Busara za Mzee Idris aliweza kuiongoza nchi kwa makini sana.

Kutokana na yote hayo yaliyokwisha kuelezwa imeonesha dhahiri kwamba Maalim Seif alikuwa mpinzani wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar tangu ASP na hatimae CCM, aidha hakuwa muumini wa kweli wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ingawa katika kauli zake mbali mbali wakati akiwa madarakani alisikika akitoa kauli kama “Mapinduzi Daima” “Udumu Muungano” “Kidumu Chama cha Mapinduzi” n.k.

Maalim Seif alipoanza kushika madaraka ya Uwaziri Kiongozi alionekana kuwa ni mtetezi wa Umma na Mwana Mapinduzi madhubuti asiyeyumba, muumini wa kweli wa Muungano na kiongozi safi wa CCM. Kumbe alikuwa mnafiki alikuwa chui aliyevaa ngozi ya Kondoo, alikuwa akicheza watu shere. Lengo lake katika kuyafanya yote hayo lilikuwa ni kujitafutia umaarufu tu, ili apate kuaminiwa na hatimae akikabidhiwa madaraka aweze kutekeleza lengo lake.

Kwa maelezo yake mwenyewe Maalim Seif, anadai kuwa yeye na kundi lake walikuwa wakiendesha siasa za Upinzani dhidi ya SMZ wakiwa kwenye Serikali na Chama cha Mapinduzi. Ndipo ilipogunduliwa njama ya Seif Shariff na kundi lake la kukihujumu Chama cha Mapinduzi, suala hili liliwasilishwa kwenye kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa na baada ya mjadala mrefu na kuthibitika kuwa Seif na wenzake wamekiuka miiko ya uwanachama na uongozi wa CCM, ndipo Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi ilipoamua kuwafukuza Uwanachama wa Chama Cha Mapinduzi Seif Shariff na wenzake wengine saba. Ambao ni Seif Sharif Hamad, Shaaban Khamis Mloo, Hamad Rashid Mohammed, Ali Haji Pandu, Masoud Omar, Soud Yussuf Mgeni, Rashid Hamadi Hamadi na Khatib Hassan Khatib

Pamoja na kuwa Chama cha Mapinduzi kimechukua hatua za kuwafukuza Uwanachama watu hao baada ya kupata uthibitisho kuwa kutokana na matendo yao hawawezi tena kuendelea kuwa Wanachama wa CCM. Lakini kundi la watu hao walipofika Zanzibar walidai kuwa awameonewa. Na Chama cha Mapinduzi katika kufikia uamuzi wake wa kuwafukuza Uwanachama awatu hao, haki haikutendeka, na kwa upande wao wahusika walikuja Zanzibar na kupita sehemu mbali mbali huku wakidai kuwa wameonewa.Tofauti na kauli aliyotoa mwenyewe Maali Seif katika moja ya hotuba yake akihutubia wanachama wa Chama chake kuwa Chama chao cha CUF kina mizizi mirefu kwani harakati zake zilianza tangu iaka ya 80 wakati wa Utawala wa Mzee Aboud Jumbe kama tunakumbuka wakati huo walianza na P.L.O (Pemba Liberation Organization), huku wenyewe wanajisifu kuwa ilifanya kazi kubwa ya kumuondoa madarakani Rais Abouid Jumbe mnamo mwaka 1984. Katika kuthibitisha kwao kuwa walikuwa wapinzani ndani ya CCM na Serikali zake wasaliti hawa mnamo mwaka wa 1988 – 1992
Walianzisha harakati za upinzani wa chini kwa chini kwanza walianza kwa kuanzisha kikundi cha “BISMILAHI’, na baadae kubadilika na kua “HAMAK”, baada ya muda mdogo tu wakabadilisha na kuwa “KAMAHURU” ambayo iliongozwa na Mwenyekiti Shaaban Khamis Mloo; Katibu Mkuu wake alikuwa Ali Haji Pandu na wajumbe wengine
walikuwa ni Soud Yussuf Mgeni, Suleiman Seif Hamad na baadhi ya wafuasi wa Maalim Seif ambao ameanza nao harakati hizi. Kikundi hiki cha upinzani kilichoongozwa na Maalim Seif kilikuwa na lengo la kupinga Uongozi wa Chamamcha Mapinduzi, Serikalia ya Mapainduzi na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ilipoingia miaka ya 1990 kilijigeuza jina na kuwa ZUF, (Zanzibar United Front). Kwa kuwa upinzani kwa kipindi hicho ndani ya Tanzania ulikuwa bado haujaruhusiwa kisheria, ndipo Serikali za CCM ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zilichukua hatua za kuudhibiti uchochezi huo kwa kuchukuwa hatua kadhaa za kisheria, Vyombo vya dola wakati vinachukua hatua za kuwashughulikia wale wote waliodhaniwa kuwa wanavunja sheria ndipo Maalim Seif kaatika kusachiwa nyumbani kwake alikutwa na nyaraka za Serikali, nyaraka ambazo hakutakiwa kuwa nazo kwa mujibu wa Sheria kwani nyaraka hizo zilikuwa ni za siri za Serikali wakati yeye sio Kiongozi tena wa Serikali. Kutokana na kadhia hiyo Seif Shariff ilibidi kufunguliwa mashitaka kutokana na kosa la kukutwa na nyaraka za siri za Serikali.

Pamoja na kufunguliwa mashitaka Mahakamani. Baada ya Maalaim Seif kufikishwa Mahakamani na kusomewa shitaka lake, Serikali ilibidi kuendelea na uchunguzi na ili mshtakiwa asije akapoteza ushahidi Mahakama iliamua kumnyima dhamana mshitakiwa na kuwekwa rumande kwa muda usiopungua miaka 30 sawa na mwaka mmoja na nusu.

Wakati Seif Sharif akiwa Mahabusu huku nyuma wafuasi wake waliendeleza uhasidi na ufisadi dhidi ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Waliendelea kutumia mali za Serikali na kwa Pemba waliendesha Kampeni kuhakikisha kila mzaliwa wa Pemba lazima akubaliane na matakwa yao. Mbinu walizozitumia katika kuwafanya watu wa Pemba wakubaliane nao ni kuzua uongo kuwa kiongozi wao amewekwa kizuizini na kubambikizwa kesi isiyokuwa ya kweli, watu wa Pemba wanaonewa na watu wa Unguja na Zanzibar inamezwa na Tanzania Bara. Kwa hivyo walianzisha kampeni za kuwachochea wananchi kudai kura ya maoni juu ya muundao wa Muungano, eti kwa sababu wakati ulipoanzishwa. Suala la kura ya maoni lilikuwa ndio sera yao, wachochezi hawa wa chini kwa chini waliliremba na kulipaka mafuta na hatimae likawa linazungumzwa kwenye vikundi vyao kila wanapokutana. Wachochezi hawa kwa kuwa walikuwa wanataka kuyateka mawazo ya watu wa Zanzibar ilibidi kuwambia uongo kuwa Muungano unaikandamiza Zanzibar na kwa kuwa Zanzibar ilikuwa inakabiliwa na hali ngumu ya Kiuchumi kutokana na kushuka bei ya zao la karafuu, zao ambalo lilikuwa ndio zao pekee lililotegemewa kwa uchumi wa Zanzibar. Basi suala la hali ngumu ya uchumi wa Zanzibar moja kwa moja likanasabishwa na Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwa hivyo wachochezi hawa wakaanza kazi ya kuwachochea Wapemba kwa kuwaambia kuwa wanaonewa na Waunguja. Na wanapokuwa Unguja waliwaambia watu wa Unguja kuwa Tanzania Bara imeimeza Zanzibar kupitia Muungano na hali ndio maana imekuwa ngumu katika uchumi na maendeleo ya jamii. Wachochezi hawa wanapokuwa Tanzania Bara walikuwa wanawaambia Watanzania wenye imani ya dini ya Kiislamu kuwa Uislamu unapigwa vita na Serikali, walikuwa wanatoa vigezo kama cha Waislamu kuwa nyuma ki-elimu, kuwa na idadi ndogo ya viongozi wenye imani ya kiislamu katika Wizara za Serikali na vyombo vya Dola, jambo ambalo lilipelekea kujitikeza baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu kuwa na misimamo mikali ya kidini na kuanza kupambana na vyombo vya Dola. Mfano uliyo hai ni matukio mawili ya vurugu zilizoanzishwa na wafuasi hao kuhusiana na Dini, moja ni lile la maandamano ya kidini yaliyofanywa hapa Zanzibar kwa kudaiwa kupinga kauli ya kiongozi mmoja wa UWT kudai wanawake waolewe na mume zaidi ya mmoja. Maandamano mengine ni yale yaliyofanyika mjini Dar es Salaam katika Mtaa wa Magomeni Mwembechai yanayodaiwa yamefanyika kupinga kuuzwa nyama za Nguruwe katika Mabucha.

Maandamano yote hayo yaliyofanyika Zanzibar na Dar es Salaam yalikuwa hayana mnasaba na Dini bali lengo lilikuwa ni kuendesha upinzani dhidi ya Chama cha mapinduzi na Serikali zake. Sababu kubwa iliyopelekea maandamano hayo kuonekana kuwa si maandamano ya kidini ni kuwa, waandamanaji waliamua kupiga askari wa vyombo vya Ulinzi wa nchi yetu, kuvamia Afisi za Chama cha Mapinduzi na kuharibu mali za Serikali kama magari Afisi na kadhalika. Katika Uchaguzi Mkuu wa Serikali wa mwaka l990, Maalim Seif na kundi lake walielekeza nguvu zao Pemba kwa kufanya kampeni ya kuwazuwia wananchi wasijiandikishe kuwa wapiga kura. Na kama inavyoeleweka kwa mujibu wa Sheria za Uchaguzi mwananchi kma hakujiandikisha kuwa mpiga kura basi anakuwa amepoteza haki yake ya kupiga kura. Kama kawaida yao, walipoona kampeni yao haiungwi mkono na wananchi wengi walianzisha mtindo wa kutumia vitisho dhidi ya wale wote walioonyesha kukaidi amri yao ya kutokwenda kujiandikisha. Wananchi walitishwa kwa kuambiwa akuwa atakaekwenda kujiandikisha basi adabu yake ni kugomewa. Wale walioonekana kuwa na msimamo tofauti waliviziwa njiani walipokuwa wanatoka katika vituo vya kujiandikisha na kunyang’anywa Kadi zao za kujiandikisha. Kwa wale wananchi walioamua kutumia haki yao ya kujiandikisha, iliwalazimu kujiandikisha kwa njia za kificho ili wasijulikane kuwa wamejiandikisha, iliwalazimu kujiandikisha kwa njia za kificho ili wasijulikane kuwa wamejiandikisha. Na wale wote waliobainika kuwa wamejiandikisha walisusiwa,walipakiwa kinyesi nyumba zao, wengine nyumba zao zilitiwa moto, waling’olewa mazao yao mashambani, mashamba yao ya Mikarafuu yalitiwa moto, wanawake waliachwa na waume zao na wanaume wameachishwa na wake zao. Wachochezi hao walidiriki hata kuvihujumu vituo vya kujiandikisha wapiga kura kwa kuvipaka kinyesi cha binadamu na hata kuvichoma moto. Matukio haya yalisababisha uandikishaji wa wapiga kuraa katika Uchaguzi Mkuu wa 1990 kwa upande wa Pemba kutokufanikiwa vizuri, kwani wananchi wengi hawakuweza kujiandikisha. Waliojiandikisha wengi wao ni wale wananchi waliojitolea muhanga pamoja na wengi wa Watumishi wa Serikali tu.

Matukio haya ya upinzani wa chini kwa chini na kubakia na baadhi ya viongozi bdabi ya Chama na Serikali ambao wanashirikiana na wapinzani katika kupinga na kuleta hujuma kwa Serikali, huenda ikiwa ni miongoni mwa sababu iliyopelekea Chama cha Mapinduzi kuamua kuanzisha mfumo wa Vyama vingi vya Siasa nchini ili kuondoa shari licha ya mfumo huo kupingwa na wananchi walio wengi kama ilivyoelezwa na Tume ya Nyalali. Dhana ilikuwa ni kwamba ukianzishwa mfumo huu wapinzani hao hawatokuwa na sababu tena ya kuendesha siasa za uhasama na kwamba utajitokeza utamaduni wa kupingana bila kupigana, kutofautiana bila kugombana. Lakini lililojitokeza kwa wapinzani hao ni kinyume kabisa na lengo lililokusudiwa. Kutokana na kuonekana kuwa wana ajenda yas siri ambayo haiwafikiani na taraatibu za kidemokrasia. Ndipo CCM ilipoamua kwa makusudi kuanzisha Mfumo wa Vyama vingi vya Siasa nchini. Kwa kipimo chochote kile, Tanzania imejitahidi mwisho wa kikomo chake kuingiza nchini Mfumo wa Vyama vingi. Na ikatoa nafasi kwa vyama mbali mbali kujitokeza na kuchangia katika utaratibu huu na wakati huo huo ikafaulu kudumisha amani na mshikamano wa Kitaifa. Imefikia mahali ambapo Tanzania iliwaachilia wananchi waamue wenyewe juu ya mustakabali wao wa kisiasa.

Baada ya kukubaliwa kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini, na kutolewa masharti ya aina ya vyama vinavyokubalika. Kikundi kilichokuwka cha uchochezi cha ZUF (Zanzibar United Front) kilichokuwa kikionbgozwa na Bwana Shaaban Khamis Mloo akiwa Mwenyekiti wa Bwana Ali Haji Pandu Katibu Mkuu wake, waliungana na Chama cha Wananchi cha Bwana James Mapalala na kuunda chama akilichoitwa Civic United Fron (CUF) ili kupata Chama cha Kitaifa. Kabla kikundi hiki cha ZUF kilikuwa na lengo la kujigeuza kuwa Chama cha Siasa bila ya kuungana na kikundi chochote kutoka Tanzania Bara. Kwani kikundi hiki hakikuwa na haja ya kupata wafuasi kutoka Tanzania Bara, kwani lengo lake lilikuwa ni Zanzibar pekee. Kujiunga kwake na kikundi cha Bwana James Mapalala ilikuwa ni mkakati tu, wa kupata Usajili wa Chama chao.

Baada tu, ya kupata usajili Chama cha CUF, wafuasi wake wakacharuka kuweka bendera kila pahali jambo ambalo lilikuwa ni kinyume cha Sheria na taratibu za nchi. Maalim Seif akiwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho, alianza kupeperusha bendera kwenye gari yake na kujifanya kuwa sawasawa na Rais wa nchi.

No comments: